Showing posts with label kitaifa. Show all posts
Showing posts with label kitaifa. Show all posts
Wednesday, September 17, 2014
Tuesday, September 9, 2014
Picha 3 za kituo cha Polisi kilichovamiwa Geita alafu Polisi wawili wakauliwa na watu wenye silaha.

Nilisoma moja ya gazeti lililokua limeandikwa IGP atangaza dau la milioni 10 kwa yeyote atakaefichua wanaohusika na uvamizi wa kituo cha Polisi ambao pia walifanya mauaji ya Polisi wake wawili Bukombe Geita.

Baadhi ya mashuhuda wamekubali kuzungumza na akiwemo mlinzi ambae anafanya kazi eneo jirani na kituo hiki anaesema ‘Ilikua kitu kama saa tisa na dakika 40 niliona magari yanapitapita pamoja na pikipiki, kama muda wa dakika 5 nikasikia kitu kama tairi kimepasuka hisia yangu kwavile ni mlinzi mzoefu nilishtuka nikasema mbona hilo sio tairi manake gari sikuiona, kidogo tena nikasikia mengine yanapigwa kama mara tatu’
‘Vibunduki vidogo vikawa vinapigwa chapchap tu nikaanza kushangaa na kuanza kujifichaficha kukimbia huku na huku, ilipofika saa mbili tukakuta watu wawili wameuwawa Mwanamke mmoja na Mwanaume mmoja wametupwa kwenye mtaro barabarani, matukio kama haya yameshajitokeza mengi tu Geita mwingine amenyongwa tu barabarani lakini tuna muda mrefu hatukuyaona/kuyasikia’

Wakati tukisubiria ripoti nyingine ya Polisi kuhusu hili tukio unaweza kuwasikiliza mashuhuda wenyewe hapa chini.
Chanzo: millardayo.com
Saturday, September 6, 2014
Majambazi yavamia kituo cha polisi yapora silaha na kuua wilaya ya Bukombe.

Watu wanaosadikika kuwa ni majambazi wamevamia kituo cha polisi wilaya ya bukombe na kuua askali polisi wawili na kujeruhi askali wengine wawili.
Akizungumza na waandishi wa habari, mkuu wa jeshi la polisi Igp Ernest Mangu amesema majambazi hao walivamia kituoni hapo saa nane usiku ambapo walirusha mabomu na kuua askali wawili, waliouwawa ni wp 7106 Uria Mwandiga na g 2615 Dastani Kimati waliojeruhiwa ni h627 Mohamedi Hassani na cpl 5131 David Ngupama.
Igp Mangu amesema katika uvamizi huo silaha mbalimbali zimeibiwa ambapo jeshi la polisi limetangaza zawadi ya shilingi millioni kumi kwa yeyote atakayefanikisha kukamatwa kwa wahalifu hao na silaha zilizoibiwa.
Akithibitisha kupokelewa kwa majeruhi na miili ya marehemu mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Bukombe daktari Honaratha Rutatinsibwa amesema hali za majeruhi ni mbaya na wamehamishiwa katika hospitali ya rufaa Bugando.
Watu 36 wamefariki 79 wajeruhiwa kaitka ajali Musoma.



Watu 36 wamefariki dunia papohapo na wengine 79 kujerihiwa vibaya katika ajali mbaya ambayo imetokea saa tano leo asbuhi katika kijiji cha sabasaba nje kidogo ya mji wa musoma wilaya ya butiama mkoani mara kwa kuhusisha mabasi mawili ya abiria na gari dogo aina ya Nissani Tellono yenye namba za usajili T332 AKK.
Mbali na gari hilo kugongwa na kutumbukia ndani ya mto mmoja katika daraja hilo kwenye barabara kuu ya Musoma –Mwanza pia mabasi mawili ambayo yamehusika katika ajali mbaya ni j4 express yenye namba za usali T677 CYC liyokuwa ikitokea jijini Mwanza kwenda sirari wilayani tarime ambalo limegongano uso kwa uso na basi la Mwanza coach yenye namba T736 AWJ lilokuwa likitokea Musoma kwenda jijini Mwanza.
Baada ya taarifa za ajali kusambaa katika manipaa ya musoma vilio na simanzi vimetawala katika mji huo wa Musoma mkoani Mara baada majeruhi na miili ya marehemu wa ajali hiyo kuanza kufikishwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mara mjini Musoma.
Wakizungumza wakati wakipatiwa matibabu baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo wamesema kuwa ajali hiyo imesababishwa na mwendo kasi wa mabasi hayo hatua ambayo ilisababisha kushindwa kupishana katika daraja hilo hivyo kugongana uso kwa uso.
akizungumza kwa niaba ya mganga mkuu wa mkoa wa Mara Dk Martin Khan,amesema kuwa wamepokea maiti na idadi kubwa ya majeruhi na wengi wao hali zao si za kuridhisha.
Hata hivyo Dk Khan ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kujitolea damu kwani amesema kuwa hospital hiyo ya rufaa ya mkoa wa mara inakabiliwa na upungufu mkubwa wa damu katika kuhudimia wagonjwa wakiwemo majeruhi wa ajali.
kamanda wa polisi mkoa wa Mara ACP Alex Kalangi, akizungumza na ITV kwa njia ya simu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba taarifa rasmi za jeshi la polisi zitatolewa baada ya kupata taarifa kutoka kwa madaktari na kwamba ametoa wito kwa wananchi kujitokea katika hospitali ya mkoa kwaajili ya kutambua miili ya marehemu.
Rais Kikwete atoa nishani kwa wanajeshi 59 wa jeshi la ulinzi la wananchi wa Tanzania.
.jpg)
Amiri jeshi mkuu rais Jakaya Kikwete ametoa nishani kwa askari hamsini na tisa wa jeshi la ulinzi la wananchi wa Tanzania wakiwemo askari wastaafu waliyofariki dunia na waliyopo kazini wakiongozwa na mkuu wa majeshi jenerali Davis Mwamnyange.
Katika tukio hilo lilifanyika kwenye chuo cha maafisa wa jeshi Monduli rais Kikwete alianza kwa kuwavavisha nishani mkuu wa majeshi jenerali Davis Mwamnyange na mnadhimu mkuu wa jeshi luteni jenerali Samweli Ndomba.
Wakizungumza baada ya kutunukiwa nishani hizo zikiwemo nishani za operasheni safisha msumbiji na nishani ya kumbukumu ya miaka hamsini ya jeshi la ulinzi la wananchi wa Tanzania askari wastafu akiwemo brigedia jenerali Hasani Ngwilizi amesema askari wastaafu wamefarijika kuona jeshi bado linawajali na waliyopo kazini wasema nishani hizo zimewaongezea ari ya kutekeleza majukumu yao katika jeshi huku wawakilishi wa askari waliyofariki dunia wakiitaka serikali iendelee na utamaduni wa kuzikumbuka familia za watu waliyotoa mchango mkubwa kwa taifa.
Tukio hilo pia lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo rais mstaafu wa awamu ya pili mzee Alli Hasani Mwinyi waziri mkuu Mizengo Pinda mawaziri wakuu wastafu Edward Lowasa na mzee John Malechela pamoja na mawaziri wa serikali ya awamu ya nne.
Chanzo - IPP Media
Monday, August 18, 2014
SERIKALI YAJIZAJITITI KUSIMAMIA HAKI ZA MTOTO NA MAREKEBISHO YA TABIA.


Baadhi
ya waandishi wa habari wakiwasikiliza wawasilishaji toka Wizara ya Afya
na Ustawi wa Jamii katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) leo
Jijini Dar es Salaam.
(Picha na Frank Mvungi)
Na Frank Mvungi
Serikali
imejizatiti katika kutekeleza mpango wa majaribio wa marekebisho ya
tabia kwa watoto walio katika mkinzano na sheria na walio katika hatari
ya kukinzana na sheria katika jamii.
Hayo
yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Afisa Ustawi wa Jamii Mkuu toka
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii bw. Steven Gumbo wakati wa mkutano na
waandishi wa habari.
“Serikali imefanikiwa kukamilisha kanuni za mahabusu za watoto, makao ya watoto na shule ya maadilisho” alisema Gumbo.
Pia hatua nyingine ni kukamilika kwa miongozo ya utoaji wa huduma katika mahabusu za watoto na shule ya maadilisho.
Hatua
nyingine ni kuwepo kwa mwongozo wa kijamiii (CRP) wa Marekebisho ya
tabia kwa watoto walio katika mkinzano na sheria na walio katika hatari
ya kukinzana na sheria.
Mafanikio
mengine ni kuwajengea uwezo watumishi wote wa mahabusi za watoto na
shule ya maadilisho juu miongozo mbalimbali iliyotolewa ya kuboresha
huduma katika Taasisi hizo.
Akieleza
zaidi Gumbo amesema kwa mujibu wa sheria ya mtoto, wanaokinzana na
sheria na ambao hawajapata dhamana kutoka katika mahakama wanapaswa
kupelekwa katika mahabusi za watoto, pale ambapo mahakama imejiridhisha
kuwa mtoto huyo ametenda kosa huamuru apelekwe katika shule ya
maadilisho.
Wizara
ya Afya kupitia idara ya Ustawi wa jamii imekuwa ikishirikiana na wadau
mblimbali kama vile Polisi, Mahakama, Magereza, Tume ya Haki za
Binadamu na Utawala Bora pamoja na mashirika mbalimbali ya Kitaifa na
Kimataifa katika kufanikisha na kutekeleza majukumu yake.
Watoto
wanaokinzana na sheria wanatunzwa katika mahabusi tano za watoto
zilizopo katika mikoa ya Tanga, Arusha, Kilimanjaro, Mbeya na Dar es
salaam na katika shule ya maadilisho ya Irambo-Mbeya.
PINDA AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA BARABARA WA TAMISEMI
Waziri
Mkuu. Mizengo Pinda akisalimiana na Katibu Mkuu , Ofisi ya Waziri Mkuu,
TAMISEMI, Jumanne Sajini baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Kilimanjaro August 17, 2014 na atafungua Mkutano wa
Wadau wa barabara wa Serikali za Mitaa kwenye hoteli ya Ngurdoto
Arusha August 18, 2014. Katikati ni Waziri wa TAMISEMI , Hawa Ghasia.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


WAZIRI GAUDENSIA KABAKA AIPONGEZA TPB KUTOA MIKOPO KWA WASTAAFU

Kutoka
kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta (TPB), Sabasaba
Moshingi, Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka na baadhi ya
viongozi meza kuu wakiwa wameshikana mikono na kuinyanyua juu ikiwa ni
ishara ya kuwaunganisha wastaafu kwenye fursa mara baada ya uzinduzi wa
mpango maalumu wa kutoa mikopo kwa wastaafu wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF
leo jijini Dar es Salaam.

Waziri
wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka akizungumza katika uzinduzi wa
mpango maalumu wa kutoa mikopo kwa wastaafu wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF
leo jijini Dar es Salaam.

Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi akizungumza katika
hafla ya uzinduzi wa mpango maalumu wa kutoa mikopo kwa wastaafu wa
Mfuko wa Pensheni wa LAPF leo jijini Dar es Salaam.

Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi (kushoto)
akimkaribisha Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka meza kuu mara
baada ya waziri huyo kuzinduwa rasmi mpango maalumu wa kutoa mikopo kwa
wastaafu wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF leo jijini Dar es Salaam.

Waziri
wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka (wa nne kulia), Ofisa Mtendaji Mkuu
wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi (wa tano kulia) wakiwa katika picha
ya pamoja na baadhi ya wageni waalikwa walioshiriki katika mpango
maalumu wa kutoa mikopo kwa wastaafu wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF leo
jijini Dar es Salaam.

Baadhi
ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa mpango maalumu
ulioandaliwa na Benki ya Posta (TPB) wa kutoa mikopo kwa wastaafu wa
Mfuko wa Pensheni wa LAPF leo jijini Dar es Salaam.

Baadhi
ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa mpango maalumu
ulioandaliwa na Benki ya Posta (TPB) wa kutoa mikopo kwa wastaafu wa
Mfuko wa Pensheni wa LAPF leo jijini Dar es Salaam.

Baadhi
ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa mpango maalumu
ulioandaliwa na Benki ya Posta (TPB) wa kutoa mikopo kwa wastaafu wa
Mfuko wa Pensheni wa LAPF leo jijini Dar es Salaam.
WAZIRI
wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka ameipongeza Benki ya Posta Tanzania
(TPB) kwa kuandaa mpango maalumu wa kutoa mikopo kwa wastaafu wa Mfuko
wa Pensheni wa LAPF ikiwa ni fursa itakayowainua kiuchumi wastaafu hao.
Waziri Kabaka ametoa pongezi hizo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizinduwa rasmi mpango wa mikopo kwa wastaafu wa Mfuko wa Penseni wa LAPF, mpango utakaowawezesha wastaafu sasa kuchukua mikopo na kuendelea kukidhi maitaji yao kipindi hicho. Akizungumza kabla ya uzinduzi huo, Waziri Kabaka alisema Benki ya Posta na Mfuko wa Penseni wa LAPF hauna budi kupongezwa kwa hatua ya kulikumbuka kundi la wastaafu ambalo kimikopo lilikuwa limesahaulika.
Waziri Kabaka ametoa pongezi hizo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizinduwa rasmi mpango wa mikopo kwa wastaafu wa Mfuko wa Penseni wa LAPF, mpango utakaowawezesha wastaafu sasa kuchukua mikopo na kuendelea kukidhi maitaji yao kipindi hicho. Akizungumza kabla ya uzinduzi huo, Waziri Kabaka alisema Benki ya Posta na Mfuko wa Penseni wa LAPF hauna budi kupongezwa kwa hatua ya kulikumbuka kundi la wastaafu ambalo kimikopo lilikuwa limesahaulika.
“…Naomba
nichukue nafasi hii kuwashukuru Benki ya Posta Tanzania pamoja na Mfuko
wa Pensheni wa LAPF kwa kubuni mpango huu maalum wa kuwasaidia wastaafu
kimaisha na kuwawezesha kumudu gharama za mahitaji yao na kukabiliana
na ukosefu wa muda mfupi wa fedha wanazohitaji kwa kuwapatia mikopo,”
alisema Waziri Kabaka.
Aliongeza
kuwa mpango huo utawasaidia wastaafu kipindi cha maisha yao mapya ya
kustaafu kwani licha ya muda huo wengi kuwa na kipato kidogo cha mapato
lakini gharama za maisha kwao hazipungui na badala yake huendelea
kupanda, jambo ambalo lilikuwa changamoto kubwa kwao.
“…Ninafarijika
kuona kwamba Benki ya Posta pamoja na LAPF mmeliona hili na kulifanyia
kazi, na hatimaye kuja na huduma hii ya mikopo. Lengo mahususi la mpango
huu ambao kwa kiasi fulani umeanza kutekelezwa ni kuwapa faraja na
kuwasaidia wastaafu katika kukidhi mahitaji yao mbalimbali, ili kuweza
kuboresha maisha yao na maslahi kwa ujumla,” alisema waziri huyo.
Kwa upande wake, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi akizungumza katika hafla hiyo, alisema mkopo huo ni wa kwanza na wa aina yake katika soko la mabenki nchini hivyo wanaamini utatoa hauweni kwa wastaafu wa LAPF.
Akifafanua zaidi alisema mstaafu anayehitaji kuwa na dhamana huku riba inayotozwa kwa mkopo huo kuwa ni ndogo yaani asilimia 12 tu kwa mwaka ukilinganisha na mikopo mingine. “…Mkopo huu umewekewa bima, hivyo endapo mkopaji atafariki familia yake haitaendelea kudaiwa. Hivyo wastaafu wote wa mfuko wa LAPF wanaweza kupata mikopo hii ambayo marejesho yake ni kati ya mwaka mmoja hadi miaka mitatu,” alisema Moshingi.
Kwa upande wake, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi akizungumza katika hafla hiyo, alisema mkopo huo ni wa kwanza na wa aina yake katika soko la mabenki nchini hivyo wanaamini utatoa hauweni kwa wastaafu wa LAPF.
Akifafanua zaidi alisema mstaafu anayehitaji kuwa na dhamana huku riba inayotozwa kwa mkopo huo kuwa ni ndogo yaani asilimia 12 tu kwa mwaka ukilinganisha na mikopo mingine. “…Mkopo huu umewekewa bima, hivyo endapo mkopaji atafariki familia yake haitaendelea kudaiwa. Hivyo wastaafu wote wa mfuko wa LAPF wanaweza kupata mikopo hii ambayo marejesho yake ni kati ya mwaka mmoja hadi miaka mitatu,” alisema Moshingi.
Alisema
huduma za mikopo hiyo ni za haraka na bora na zitatolewa kwa matawi
yote ya Benki ya Posta Tanzania hivyo kuwataka wahitaji wote wastaafu wa
Mfuko wa Penseni wa LAPF kwenda katika matawi hayo popote nchini kupata
maelezo ya nini cha kufanya kabla ya kupata mkopo huo.
Hata
hivyo TPB kwa kushirikiana na LAPF wamezishauri taasisi za fedha
nyingine zikiwemo Benki kuangalia namna ya kuweka mipango ya kusaidia
wastaafu nchini kwani kundi hilo lina kiasi kikubwa cha fedha ambacho
kikitumiwa vyema kinaweza kuleta mchango mkubwa katika uchumi wan chi ya
Tanzania. Hafla hiyo pia iliyohudhuriwa na viongozi waandamizi na
wafanyakazi wa TPB na Mfumo wa Penseni wa LAPF ilishirikisha pia baadhi
ya wastaafu ambao baadhi walieleza wameanza kunufaika na mpango huo wa
mikopo kwa wastaafu.
*Imeandaliwa na www.thehabari.com
*Imeandaliwa na www.thehabari.com
Sunday, April 20, 2014
Ukawa ruksa kufanya mikutano nchi nzima
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda ametoa ruksa kwa wanachama wanaounda Umoja wa
Katiba ya Wananchi (Ukawa) kufanya mikutano yao nchi nzima. Pinda
alizungumza jana wakati akifunga maonyesho ya miaka 50 ya Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es
Salaam, alisema yaliyotokea bungeni yanaweza kumalizika kwa kukaa meza
moja ya majadiliano.“Yale
mambo ya bungeni yanaweza kumalizika na tukaendelea kama ambavyo
ilikuwa katika majadiliano ya kutengeneza kanuni. Tulikuwa
tukishindana kwa kukaa meza moja na kumalizana, kisha tunaendelea sasa hili tumeshindwa nini?” alihoji Pinda Alisema:
“Walitoka bungeni na kusema watazunguka nchi nzima, nasema wazunguke tu
kuwaeleza wananchi na sisi hatutashindwa kuzunguka kwani hoja tunazo.”Waziri
Mkuu Pinda alitumia nafasi hiyo kuelezea kauli aliyoitoa Waziri wa Nchi
Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi kwenye
Kanisa la Methodist kwamba hoja ya serikali tatu ikipita inaweza
kulifanya jeshi kuchukua madaraka.Alisema nilimpigia simu nikamweleza: “Rudi mara moja ueleze kilichotokea huko na nafikiri mlimsikia alichokisema.”Lukuvi
akitoa ufafanuzi bungeni bila ya kuwapo kwa Ukawa alisema: “Nayasema
yote haya kwa kuwa naamini huo ndio msimamo wangu na utakuwa msimamo
ambao wakati wote utaendelea kuwa hivyo na ninawataka ndugu zangu kuacha
unafiki.”Kutokana
na kauli hizo, Ukawa inayoundwa na vyama vya Chadema, CUF, DP na
NCCR-Mageuzi na wajumbe 25 kutoka kundi la 201 walitoka bungeni Jumatano
wiki hii na kuahidi kuzunguka nchi nzima kufanya mikutano ya hadhara
kuwaleza wananchi kilichotokea.chanzo mwananchi

Subscribe to:
Posts (Atom)