Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Tuesday, September 9, 2014

Picha 3 za kituo cha Polisi kilichovamiwa Geita alafu Polisi wawili wakauliwa na watu wenye silaha.


Geita Polisi 2014 2 
Nilisoma moja ya gazeti lililokua limeandikwa IGP atangaza dau la milioni 10 kwa yeyote atakaefichua wanaohusika na uvamizi wa kituo cha Polisi ambao pia walifanya mauaji ya Polisi wake wawili Bukombe Geita.
Geita Polisi 2014 3 
Baadhi ya mashuhuda wamekubali kuzungumza na  akiwemo mlinzi ambae anafanya kazi eneo jirani na kituo hiki anaesema ‘Ilikua kitu kama saa tisa na dakika 40 niliona magari yanapitapita pamoja na pikipiki, kama muda wa dakika 5 nikasikia kitu kama tairi kimepasuka hisia yangu kwavile ni mlinzi mzoefu nilishtuka nikasema mbona hilo sio tairi manake gari sikuiona, kidogo tena nikasikia mengine yanapigwa kama mara tatu’
‘Vibunduki vidogo vikawa vinapigwa chapchap tu nikaanza kushangaa na kuanza kujifichaficha kukimbia huku na huku, ilipofika saa mbili tukakuta watu wawili wameuwawa Mwanamke mmoja na Mwanaume mmoja wametupwa kwenye mtaro barabarani, matukio kama haya yameshajitokeza mengi tu Geita mwingine amenyongwa tu barabarani lakini tuna muda mrefu hatukuyaona/kuyasikia’

Geita Polisi 2014 1Shuhuda Mwanamke ambae anaeishi karibu na eneo hili anasema alikua amelala wakati tukio linatokea na alilisikia, anachoomba ni idadi ya Polisi kuongezwa kituoni hapo ili kuongeza nguvu zaidi hata 100 akisema ‘kile kituo ni kikubwa lakini askari ni wachache’
Wakati tukisubiria ripoti nyingine ya Polisi kuhusu hili tukio unaweza kuwasikiliza mashuhuda wenyewe hapa chini.

Chanzo: millardayo.com
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...