Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Saturday, September 6, 2014

Rais Kikwete atoa nishani kwa wanajeshi 59 wa jeshi la ulinzi la wananchi wa Tanzania.

Amiri jeshi mkuu rais Jakaya Kikwete ametoa nishani kwa askari hamsini na tisa wa jeshi la ulinzi la wananchi wa Tanzania wakiwemo askari wastaafu waliyofariki dunia na waliyopo kazini wakiongozwa na mkuu wa majeshi jenerali Davis Mwamnyange.
Katika tukio hilo lilifanyika kwenye chuo cha maafisa wa jeshi Monduli rais Kikwete alianza kwa kuwavavisha nishani mkuu wa majeshi jenerali Davis Mwamnyange na mnadhimu mkuu wa jeshi luteni jenerali Samweli Ndomba.
 
Wakizungumza baada ya kutunukiwa nishani hizo zikiwemo nishani za operasheni safisha msumbiji na nishani ya kumbukumu ya miaka hamsini ya jeshi la ulinzi la wananchi wa Tanzania askari wastafu akiwemo brigedia jenerali Hasani Ngwilizi amesema askari wastaafu wamefarijika kuona jeshi bado linawajali na waliyopo kazini wasema nishani hizo zimewaongezea ari ya kutekeleza majukumu yao katika jeshi huku wawakilishi wa askari waliyofariki dunia wakiitaka serikali iendelee na utamaduni wa kuzikumbuka familia za watu waliyotoa mchango mkubwa kwa taifa. 
 
Tukio hilo pia lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo rais mstaafu wa awamu ya pili mzee Alli Hasani Mwinyi waziri mkuu Mizengo Pinda mawaziri wakuu wastafu Edward Lowasa na mzee John Malechela pamoja na mawaziri wa serikali ya awamu ya nne.

Chanzo - IPP Media
 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...