Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Wednesday, July 31, 2013

Mabaraza Katiba nchini yaonywa

 
Mwenyekiti wa Tume ya Katiba, Ali Saleh Ali, amewataka wajumbe wa mabaraza ya katiba ngazi za wilaya, wasiogozwe na ‘mawazo fungwa’ wakati wa kutoa maoni yao kuhusu uboreshaji wa rasimu ya katiba.Ali ametoa tahadhari hiyo juzi baada ya kutokea mvutano mkali kati yake na baadhi ya wajumbe wa baraza la katiba wilaya ya Singida, wanaohudhiria kikao cha baraza la katiba kinachoendelea kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Wananchi mjini hapa.Mvutano huo ulisababishwa na baadhi ya wajumbe kudai kuwa mwenyekiti huyo, alikuwa akifanya utetezi mkubwa ulioonyesha kila dalili kwamba una ushawishi wa moja kwa moja wa kutaka wajumbe hao wapitishe kila kitu kilichomo kwenye rasimu ya katiba.Baada ya kubanwa, mwenyekiti Ali alisema “Wajumbe naona mmekuja hapa tayari mkiwa na ‘mawazo fungwa’ kitu ambacho kinasababisha tushindwe kuelewana”.

Bila kufafanua zaidi juu ya mawazo hayo fungwa, mwenyekiti huyo alisema kuwa kwa utaratibu, ni lazima mjumbe anayeuliza swali ni lazima ajibiwe papo hapo.Lakini kwa upande wa maoni,maoni yanachukuliwa kama yalivyo na kupelekwa mbele.Ali alisema kwa sababu kuna wajumbe waliokuja na mawazo fungwa,wanapata tabu ya kuafikiana wanapojadiliana.“Kwa kifupi ni kwamba hakuna maoni ya mjumbe yeyote yatakayoachwa au kukataliwa, mnayo fursa kubwa kila mjumbe kueleza maoni yake anayoona yatasaidia kupata katiba ya ustawi wa kizazi cha sasa na kile kijacho,”alisema.Mmoja wa wajumbe wa kikao hicho, Elia Digha, alitoa duku duku lake kuwa tume ya katiba imekuja Singida kukusanya maoni na si kutetea rasimu kama alivyoonyesha mwenyekiti.Katika hatua nyingine, asilimia kubwa ya wajumbe wa kikao waliungana na Watanzania wengine wanaopinga kuundwa Serikali tatu.
Wamedai Serikali tatu italeta madhara mengi ikiwemo gharama kubwa ya uendeshaji na pia itachangia kuzorota kwa undugu uliojengeka kwa miaka mingi.
Aidha,wamepiga kipengere cha kuruhusu wagombea binafsi kwa madai utachangia mafisadi kutumia mwanya huo kupata uongozi.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...