Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Thursday, May 2, 2013

PICHA: Semina ya wasanii waliochaguliwa kuwania tunzo za Kili mwaka huu yafana

 Jana ilifanyika semina kwa wateule wa tunzo za muziki za Kilimanjaro za msimu huu ambapo kwa mara ya kwanza, wasanii walizipongeza kwa asilimia kubwa na kutoa maoni zaidi kuliko kuzikosoa kama ilivyokuwa awali.
Katika semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa New World Cinema maeneo ya Mwenge jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa pia na viongozi wa Baraza la Sanaa la Taifa pia wasanii walipata elimu mbali mbali kuhusiana na jinsi mchakato mzima wa tunzo hizo utakavyokuwa ukiendelea.
Tunzo za mwaka huu zimebeba jina la kivyetuvyetu zikiwahimiza watanzania kupenda vya kwao, hamasa iliyowaingia wanamuziki hao ambao walionekana kutoa mawazo ya kuboresha tunzo zaidi kuliko kuzitafuta makosa huku wakiamini kwa asilimia mia moja kwamba hizi tunzo ni za kwao, na wana jukumu la kuzifanya ziwe bora kwa kufanya nazo kazi bega kwa bega.
Pichani juu ni Mzee Yusuph kulia, akiwa na wasanii kutoka katika kundi la jahazo Modern Taarab
 ...katikati ni Nikkii wa pili kutoka kundi la Weusi
 Kutoka kushoto ni Queen Darleen, mwasiti na Linah kutoka THT
 Luiza Mbutu hapa akiwa katika utani na meneja wa Mashujaa Band, Martin Sospeter(Aliyevaa Tshirt Nyeupe)
 george Kvishe, meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, wadhamini na waendeshaji wa tunzo za za muziki Tanzania akiongea machache na wasanii waliochaguliwa kuingia katika kinyang'anyiro hicho mwaka huu
 ..mnh, ..huyu nae...
 Linah, akiteta jambo na Rachel wakati mchakato ukiendelea
 Mkubwa Fella, Meneja wa makundi ya THT na Mkubwa na wanawe akitoa mawazo yake katika semina hiyo
 Malkia Khadija Kopa maye alipasha yake
 meza kuu, ...(Bisha)
 Jike la Simba, Isha Mashauzi naye alilonga yake
 Nikki wa Pili naye alipata muda wa kutoa ya moyoni
 Barnabas kutoka THT
 Rama Dee
Linex
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...