Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Sunday, April 28, 2013

Exclusive:Kesi ya Jerry Muro hatarini kuanza upya



Aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC1), Jerry Murro,akiwa chini ya ulinzi wa Asakari Polisi Dar es Salaam,Tanzania

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam kesho inatarajia kutoa uamuzi wa mgumu utakaowezesha kesi ya aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC1), Jerry Murro na wenzake wawili kudiwa umpya ama kusitishwa.

Muro na wenzake wawili, Edmund Kapama maarufu kama ‘Dokta’ na Deogratius Mugassa wanaweza kupandishwa kizimbani tena na kuanza kusikiliza upya kesi ya rushwa iliyokuwa ikiwakabili.

Kwa muujibu wa taarifa za ndani kutoka Mahakama ya rufaa zilizonaswa naHabaimpya.com ni kwamba Uamuzi huo unatokana na maombi ya Jamhuri katika rufaa ya kupinga hokumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iliyowaachia huru Muro na 
wenzake, katika kesi ya rushwa iliyokuwa ikiwakabili katika mahakama hiyo.

Ikiwa Mahakama Kuu itakubaliana na hoja na maombi ya Jamhuri, basi Muro na wenzake watalazimika kupanda kizimbani tena katika
Mahakama ya Kisutu na kesi yao itaanza kusikiliza upya, kama vile ilikuwa haijawahi kusikilizwa kabisa.

Jamhuri itaibidi iwaite tena mashahidhi wake kufika mahakamani kutoa ushahidi na kama mahakama itaridhika kuwa washtakiwa hao wana kesi ya 
kujibu, basi watalazimika kujitetea na hata kuwaita mashahidi wao kama watakuwa nao, kisha mahakama itatoa hukumu yake.

Kama Mahakama Kuu haitakubaliana na hoja na maombi ya Jamhuri, basi itaweza kuamuru usikilizwaji wa rufaa hiyo uendelee ambapo Jamhuri 
itaendelea na hoja zake nyingine za kupinga hukumu ya sasa ya Mahakama ya Kisutu. Muro na wenzake, walikuwa wakikabiliwa na mashtaka ya kula njama na kuomba rushwa ya Sh10 milioni, kutoka kwa aliyekuwa Mhasibu wa 

Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Michael Karoli Wage.

Hata hivyo Novemba 30, 2011, Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Frank Moshi katika hukumu yake, aliwaachia huru, akisema kuwa upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yao bila kuacha mashaka yoyote. Jamhuri kwa kutokuridhika na hukumu hiyo, ilikata rufaa Mahakama Kuu, ikibainisha sababu nne za kuipinga hukumu hiyo.Rufaa hiyo ilisikilizwa na Jaji Dk Fauz Twaib.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...