Mfanyabiashara
na dereva aliyekuwa akiendesha gari lenye namba za usajili T.328 BML
aina ya Land Lover Discovery na kusababisha kifo cha askari mwenye namba
WP 2492 Coplo Elikiza Nnko baada ya msafara wa Rais Jakaya Kikwete
jijini Dar es Salaam ,leo kesi yake ya tuhuma za kujipatia mali ya Tsh
milioni 30 kwa njia ya udanganyifu imeendelea tena.
Mfanyabiashara
huyo Jackson Simbo Stivin(45) alifikishwa awali mahakamni hapo
akituhumiwa kujipatia gari aina ya fuso lenye thamani ya Tsh milioni 30
ambalo ni mali ya mfanyabiashara wa mkoani Iringa Venansia Sanga. Kwa
mara ya kwanza mtuhumiwa huyo alipofikishwa Hakimu wa mahakamani hiyo ya
Mwanzo Bomani Mheshimiwa Alois Masua alisema kuwa mtuhumiwa huyo
anadaiwa kutenda kosa hilo Septemba 4 mwaka 2012 katika eneo la
Miyomboni mjini Iringa . Mheshimiwa Masua alisema kuwa mtuhumiwa huyo
baada ya kutenda kosa hilo alitoweka na kujificha katika mikoa mbali
mbali hapa nchini .
Alisema
kuwa kutokana na kufunguiliwa kwa kesi hiyo jeshi la polisi kwa
kushirikiana na mlalamikaji waliendelea kumsaka mtuhumiwa huyo bila
mafanikio na baada ya kutokea ajali iliyosababisha kifo cha askari huyo
wa usalama barabarani jijini Dar es Salaam katika msafara wa Rais
Kikwete ndipo mtuhumiwa huyo alipokamatwa baada ya picha yake kuonekana
katika vyombo vya habari .
Mtuhumiwa
huyo alikana shtaka hilo dhidi yake na mahakama kudai kuwa dhamana yake
ipo wazi na kuwa mdhamini anapaswa kusaini hati ya dhamana ya yenye
thamani ya Tsh. milioni 15 masharti ambayo yalitimizwa na wadhamini na
mfanyabiashara kesi hiyo imeahirishwa hadi Mei 9 ambapo kesi hiyo
itaanza kusikilizwa na mtuhumiwa yupo nje kwa dhamana .