Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Friday, April 26, 2013

BREAKING NEWS: GODBLESS LEMA AKAMATWA....POLISI WAVUNJA MLANGO NA KUMTIA PINGU



Baada ya mabishano ya muda mrefu nyumbani kwa kada huyu na Mbunge wa Arusha mjini na uvamizi wa Polisi wakati wa usiku wa manane, Mh. Lema alikubali kukamatwa na kuchukuliwa na gari la polisi usiku na kupelekwa kituo kikuu cha polisi Arusha yaani Central Polisi.
Kukamatwa kwake kulikuja baada ya polisi kuvunja mlango na kuingia ndani na kuendesha msako wa nguvu humo ndani .Vitu kama laptop, ipad, simu vipo mikononi mwa police.
Wananchi wengi walijitokeza ku-support mbunge wao na huenda Asubuhi wananchi wakawa wengi zaidi.


Safari ya Lema kuelekea polisi ilisindikizwa na msululu wa magari ya makada waliojitokeza kumsupport kuelekea kituo cha polisi.

Baada ya kumfikisha Lema Central police Arusha alisachiwa na kuingizwa ndani. Lema alikuwa ameambatana na magari ya wafuasi wa Chadema waliomsindikiza ili kushuhudia kinachojili hapo kituoni.

Baada ya kumtupa ndani,polisi waliwafukuza wafuasi hao wa Chadema hapo kituoni na kuwaambia hawatakiwi kuonekana hapo.
.......

MH. LEMA AMEKAMATWA KUFUATIA KILE KINACHOTAJWA NA MKUU WA MKOA WA ARUSHA KUWA YEYE NDO CHANZO CHA VURUGA NA KUZOMEWA KWAE NA WANAFUNZI ALIPOFIKA CHUO CHA UHASIBU NJIRO BAADA YA TUKIO LA KINA MMOJA ALIYEUAWA KWA KUCHOMWA KISU.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...