Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Monday, July 15, 2013

HIVI NDIVYO WAHALIFU NCHINI IRAN WANAVYOKIONA CHAMOTO..

Picha mbalimbali zikionesha utekelezwaji wa adhabu ya kukatwa vidole mhalifu.
Imepigwa picha kwa mara ya kwanza kabisa, hiki ni chombo cha kinyama kinachotumiwa na mamlaka za Iran kukata vidole vya wahalifu wenye hatia.

Wanaume watatu wenye skafu wanaoneshwa wakitumia mashine chafu ya kusagia kutekeleza adhabu hiyo ya kikatili, iliyotolewa chini ya sheria kali nchini humo ya Sharia, dhidi ya mwizi aliyepatikana na hatia na mbakaji.
Mwanaume huyo aliyefunikwa macho, ambaye alipatikana na hatia katika mahakama huko mji wa kusini-magharibi wa Shiraz, anaonekana akiongozwa kuelekea kwenye chombo hicho, ambacho kinaweza kuwa kimechukuliwa kutoka katika duka la mbao.
Wanaume watatu wenye skafu kisha wakamvuta mtu huyo na mkono wake kufungwa sehemu inayotakiwa kwenye mashine hiyo.
Huku mtu mmoja akiendesha gurudumu, mashine hiyo ya kikatili inafanya kazi yake na kisha mkono wa mtu huyo unainuliwa kuonesha damu inayochuruzika kabla ambao baadaye unatumbukizwa kwenye madini joto ghafi.

Katika namna ya ajabu sura ya mtu huyo inaonesha kutohisi maumivu kushawishi kwamba inawezekana alinyweshwa dawa au kupewa ganzi kabla ya mchakato huo.
Kufuatia ukataji viungo huo, mwendesha mashitaka alitangaza kwamba adhabu za uhalifu kama hizi zinaweza kuwa kali zaidi.
Chini ya sheria za Sharia, ukataji viungo, kuchapwa mijeledi, na pengine kifo kwa kupigwa mawe zote ni aina ya hukumu za kisheria.
Picha hizi zilisambazwa na shirika la habari la nchi hiyo huku Iran ikijiandaa kuelekea kwenye uchaguzi mwezi Juni kumbadili Rais Mahmoud Ahmadinejad ambaye atakuwa ametumikia kwa kipindi chake cha mwisho cha awamu mbili.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...