Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Showing posts with label ukatili. Show all posts
Showing posts with label ukatili. Show all posts

Monday, July 15, 2013

HIVI NDIVYO WAHALIFU NCHINI IRAN WANAVYOKIONA CHAMOTO..

Picha mbalimbali zikionesha utekelezwaji wa adhabu ya kukatwa vidole mhalifu.
Imepigwa picha kwa mara ya kwanza kabisa, hiki ni chombo cha kinyama kinachotumiwa na mamlaka za Iran kukata vidole vya wahalifu wenye hatia.

Wanaume watatu wenye skafu wanaoneshwa wakitumia mashine chafu ya kusagia kutekeleza adhabu hiyo ya kikatili, iliyotolewa chini ya sheria kali nchini humo ya Sharia, dhidi ya mwizi aliyepatikana na hatia na mbakaji.
Mwanaume huyo aliyefunikwa macho, ambaye alipatikana na hatia katika mahakama huko mji wa kusini-magharibi wa Shiraz, anaonekana akiongozwa kuelekea kwenye chombo hicho, ambacho kinaweza kuwa kimechukuliwa kutoka katika duka la mbao.
Wanaume watatu wenye skafu kisha wakamvuta mtu huyo na mkono wake kufungwa sehemu inayotakiwa kwenye mashine hiyo.
Huku mtu mmoja akiendesha gurudumu, mashine hiyo ya kikatili inafanya kazi yake na kisha mkono wa mtu huyo unainuliwa kuonesha damu inayochuruzika kabla ambao baadaye unatumbukizwa kwenye madini joto ghafi.

Katika namna ya ajabu sura ya mtu huyo inaonesha kutohisi maumivu kushawishi kwamba inawezekana alinyweshwa dawa au kupewa ganzi kabla ya mchakato huo.
Kufuatia ukataji viungo huo, mwendesha mashitaka alitangaza kwamba adhabu za uhalifu kama hizi zinaweza kuwa kali zaidi.
Chini ya sheria za Sharia, ukataji viungo, kuchapwa mijeledi, na pengine kifo kwa kupigwa mawe zote ni aina ya hukumu za kisheria.
Picha hizi zilisambazwa na shirika la habari la nchi hiyo huku Iran ikijiandaa kuelekea kwenye uchaguzi mwezi Juni kumbadili Rais Mahmoud Ahmadinejad ambaye atakuwa ametumikia kwa kipindi chake cha mwisho cha awamu mbili.

Read More >>

Friday, July 12, 2013

Mama amchoma mwanaye na mkasi mara 90 kwa madai kuwa alimng’ata ziwa wakati akimnyonyesha cheki picha za mtoto huyo hapa

 
Ni kama miujiza kwa mtoto wa kichina kuwa hai mpaka sasa licha ya kuchomwa chomwa mara 90 na mama yake mzazi huko China kwa madai kuwa alimng’ata ziwa mama yake wakati akinyonyeshwa.


Kwa mujibu wa Daily Mail mtoto huyo Xiao Bao mwenye miezi 8 tu ameshonwa zaidi ya nyuzi 100 ili kuurudisha uso wake katika hali nzuri baada ya shambulizi hilo lililotokea katika jiji la Xuzhou mashariki mwa China.

Bao anaishi na mama yake pamoja na wajomba zake wawili ambao wanajishughulisha na ukusanyaji wa taka kwaajili ya kipato. Mmoja wa wajomba hao ndiye aliyegundua kuwa Bao ameumizwa baada ya kumkuta akiwa amelala kwenye damu iliyotapakaa nyumbani hapo kabla hajamkimbiza hospitali.


Mama wa mtoto huyo baadaye alikiri kumchoma choma mwanae na mkasi mara 90 hususan eneo la usoni baada ya mtoto huyo kumng’ata ziwa wakati akimnyonyesha.


Baada ya tukio hilo majirani wa familia hiyo wameiomba serikali imnyang’anye mama huyo wa kichina mtoto kwa sababu za kiusalama, lakini ombi hilo limekataliwa kwa madai kuwa hakuna uthibitisho wowote mpaka sasa kama mwanamke huyo anamatatizo ya akili, lakini wameongeza kuwa hata hivyo mtoto huyo bado ana walezi wengine wawili anaoishi nao (wajomba zake) Mtoto huyo anaendelea kupata nafuu akiwa hospitali.
Read More >>

Thursday, July 11, 2013

MWANAMKE AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MITANO JELA BAADA YA KUMTUPA MTOTO WAKE CHOONI

Mwanamke mmoja mkazi wa Manga A Jijini Mbeya amehukumiwa kifungo cha miaka 5 jela kwa kosa la kutupa mtoto wake chooni.
Tukio hilo lilitokea Juni 14, Mwaka huu katika eneo hilo baada ya watoto waliokuwa wakicheza kugundua kuwepo kwa Mtoto katika choo cha shimo.
 
Mtuhumiwa baada ya kukamatwa amekiri kutenda kosa hilo na kwamba alifanya hivyo baada ya mzazi mwenzie kumkataa.
Ameongeza kuwa amelazimika kutupa katika choo cha jirani kwa sababu ni cha shimo tofauti na chao ambacho asingeweza kutupa mtoto huyo.
  
Rukia Haruna (31)  akitolewa nje  na Askari wa Jeshi la Polisi akitolewa nje ya  Mahakama kwenda Gerezani kutumikia kifungo cha miaka 5 Jela  
 
Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Archiles Mulisa mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya, Zabibu Mpangula, amemtaja Mtuhumiwa kuwa ni Rukia Haruna (31) mkazi wa Manga A Jijini Mbeya na kwamba kosa lake ni kinyume cha kifungu  218 kifungu kidogo cha 35 sura ya 16 ya mwaka 2002.
Na  Mbeya yetu
Read More >>
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...