Omotola akiwa na mume wake na watoto.
Nuru ya Wanigeria kufanya vizuri kwenye hii dunia inazidi
kung’aa…. imekua ni kawaida sasa hivi kuona Mnigeria akifanya kolabo au
kushea stage na staa mkubwa kwenye muziki Marekani, mfano mzuri ni kina P
Square na Rick Ross, Wizkid na Chris Brown, Kanye West na D’Banj,
D’Banj na 2Chainz na wengine wengi.`
Goodnews ya sasa ni kwamba staa wa movie ambae aliwahi kuja
Tanzania kwenye uzinduzi wa movie ya kwanza ya mwigizaji Wema Sepetu,
Mnigeria Omotola Jalade ametangaza show yake ya TV ‘Hit the Floor’
kuanza kuonekana nchini Marekani June 24 2013 ambapo ndani yake
wameshirikishwa mwigizaji staa wa Hollywood Marekani Kimberly Elise na
mwimbaji staa Akon.
Ni drama series ambayo itaonekana kupitia VH1.
 |
| Kimberly Elise |
 |
| Akon |