Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Saturday, June 22, 2013

MAKINDA::MKIKATAA BAJETI BUNGE LINAVUNJWA

Spika wa Bunge Anne Makinda juzi usiku alifunga mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali, huku akiwaonya wabunge kwa kunukuu baadhi ya vifungu vya Kanuni za Kudumu za Bunge inayoashiria kuwa ikiwa hawatopitisha bajeti hiyo Rais atalivunja Bunge.
Akiahirisha kikao cha 53 cha Mkutano wa 11 wa Bunge unaoendelea mjini Dodoma juzi usiku, Spika Makinda alitaja Kanuni ya 107 (1) na (2) ambayo hutumika kukidhi matakwa ya Ibara ya 90 (2)(b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayohusu Rais kulivunja Bunge.
Kanuni hiyo ya 107.(1) inaeleza: “Mjadala kuhusu Hotuba ya Bajeti ya Serikali utakapomalizika, Spika atalihoji Bunge ili litoe uamuzi wake wa kupitisha au kutokupitisha Bajeti ya Serikali ili kukidhi matakwa ya Ibara ya 90(2) (b) ya Katiba.”
Akinukuu kifungu hicho cha Katiba, Makinda alisema: “Rais hawezi kulivunja Bunge, isipokuwa kama Bunge litakataa kupitisha bajeti.”
Mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka 2013/14 umejadiliwa kwa siku nne kuanzia Jumatatu wiki hii ambapo Makinda alisema kuwa wote walioomba kuchangia walifanya hivyo wamekwisha.
“Nafunga mjadala wa Bajeti ya Serikali Kuu leo, wote walioomba na waliokuwepo wamekwisha,” alisema Spika
Makinda.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...