Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Monday, April 29, 2013

Watu wanane wauawa katika mapambano kati ya jeshi la Algeria na watu wenye silaha

Watu wasiopungua wanane wameuawa katika mapambano kati ya jeshi la Algeria na watu wenye silaha waliokuwa wakijaribu kujipenyeza nchini humo kupitia mpaka wa nchi hiyo na Libya. 
Ndege ya upelelezi iligundua msafara wa magari manne yaliyokuwa na watu wenye silaha kujaribu kuingia Algeria kwa kuvuka mto katika eneo la mpakani. 
Mapambano hayo yalisababisha vifo vya watu watano wenye silaha na wanajeshi watatu. Jeshi la Algeria linawasaka watu wengine kumi, na kusema wengi wao ni Waalgeria na baadhi ni Watunisia. 
Hii ni operesheni kubwa kufanyika na jeshi la Algeria toka shambulizi la kigaidi lililotokea Januari wakati kisima cha kuchimba gesi cha Tiguentourine mkoani Illizi nchini humo kushambuliwa na kusababisha vifo vya wafanyakazi 37 wa nchi za nje pamoja na mwalgeria mmoja.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...