Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Monday, April 29, 2013

Mzozo wa ardhi Loliondo sasa watua kwa JK



Mzozo wa eneo tengefu la pori la Loliondo Wilayani Ngorongoro katika Mkoa wa Manyara, sasa limetua kwa Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya kupata ufumbuzi. Siku za karibuni, mzozo kati ya wakazi wa eneo hilo na Serikali uliibuka baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki kutangaza Serikali kuchukua ekari 1,500 na kuwaachia wakazi wa eneo hilo kumiliki ekari 2,500 hatua waliyoikataa. 
Katika mikutano yake na waandishi wa habari mwishoni mwa Machi na mwanzoni mwa mwezi huu, Waziri Kagasheki alishikilia msimamo wa Serikali kuwa uamuzi uliotolewa na wizara yake ni sahihi na hautabadilika.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Elias Ngolisa akitoa taarifa ya mkutano wao na Waziri  Mkuu, Mizengo Pinda katika mkutano wa hadhara uliofanyika juzi, Kijiji cha Arash, wilayani Ngorongoro, alisema baada ya kutoa maelezo yao na vielelezo, Waziri Mkuu aliahidi kupeleka mgogoro wao kwa Rais Kikwete kwa kwa ajili ya kutolea uamuzi.
“Kama ambavyo mlitutuma, tulikutana na waziri mkuu na viongozi wengine, ikiwepo Tume ya CCM na tumemweleza waziri mkuu kwa nini tunapinga agizo la Waziri Kagasheki.
Habari na Mussa Juma, Mwananchi
Chanzo - Mwananchi
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...