Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Sunday, April 28, 2013

BREAKING NEWS...IRINGA SI SHWARI MVUTANO KATI YA MACHINGA NA POLISI WATISHIA USALAMA

Machinga wakiendelea na  shughuli zao kama kawaida  eneo la mashine  Tatu asubuhi  hii kutokana na kauli  ya mbunge Msigwa kuwaruhusu kurejea ,chini polisi  wakiwa eneo hilo


Hali  si  shwari katika Manispaa ya Iringa baada ya kauli   mbunge  wa  jimbo hilo Mchungaji Peter Msigwa (Chadema) kuwataka wafanyabiashara  wadogo wadogo (machinga) kurejea kufanya kazi katika eneo la barabara  ya Mashine  tatu kutekelezwa na machinga  hao.
Msigwa ambae  aliitoa kauli hiyo April 23 mwaka  huu katika mkutano wa wabunge wa chadema  waliosimamishwa  bungeni ,mkutano  uliofanyika katika uwanja  wa Mwembetogwa  mjini hapa,kwa  kuwataka Machinga  kurejea  eneo hilo na iwapo mtu atafika  kuwanyanyasa  basi wana----!!!?
Machinga  hao  leo  wameitikia kauli  hiyo kwa  kurejea  eneo hilo na kupelekea askari  wa  kutuliza ghasia (FFU) kutanda  eneo hilo na kushindwa  kutumia nguvu zaidi ya  kuwataka wafanyaiashara hao  kuendelea na shughuli  zao  eneo hilo .

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...