Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Monday, April 15, 2013

Askofu Malasusa achangisha Milioni 64/-, Sitta anunua kuku kwa Mil.1/-

 
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dkt. Alex Malasusa, jana Aprili 15, 2013 amechangisha zaidi ya Milioni 64/- katika Harambee ya Ujenzi wa Kanisa la Usharika wa Mpwapwa, ambapo WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, alinunua Tenga la Kuku kwa Shilingi Milioni Moja.
Sitta akiwa miongoni mwa wabunge waliopigiwa simu na Askofu Dkt. Malasusa ili kuwajulia hali kutokana na majukumu ya kitaifa ya Bunge waliyonayo mjini Dodoma, aliitikia wito wa Baba Askofu Malasusa na akamuunga mkono kwa kununua Tenga la Kuku kwa Milioni Moja Taslimu.
Aidha Katika changizo hilo, Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Christopher Kangoye alichangia Shilingi Milioni 1.5/-, katika Harambee hiyo ambayo Askofu Malasusa pamoja na mambo mengine alichangisha zaidi ya Milioni 64/=.
Kwa upande wa waumini kila aliyechangia Harambe na kutaka kupiga picha na Mkuu wa KKKT Askofu Malasusa, alijikuta akifunguliwa mioyo na kupiga naye picha Moja kwa Shilingi Laki 5/-, tofauti mahali pengine ambapo hupiga naye picha kwa Shilingi 50/-.
Tunu na Baraka ya pekee ilikuwa ni kwa Mtoto aliyebatizwa papo kwa papo, huku wazazi wake wakiridhia kufunga Harusi (Pingu za Masha) ingawa walipoamka asubuhi hawakuwa na lengo wala ndoto za kufunga Ndoa siku hiyo.
Kwa muujiza huo, Askofu Mkuu wa Dayosisi ya KKKT Dodoma Amoni Kinynyu alisema, vyeti vya wana ndoa hao zitasubiri siku 21 za tangazo la ndoa kuona iwapo kutakuwa zuio lolote la harusi yao kisheria na zitakapomalizika bila zuio watakabiddhiwa shahada zao.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Jimbo la KKKT Mpwapwa na ambaye ni Mchungaji wa Usharika huo, amesema wakusudia kukusanya zaidi ya Milioni 100/- lakini kwa mafanikio hayo wamemshukuru Mkuu wa KKKT Askofu Dk. Malasusa amewasaidia kwa kiasi kikubwa na jimbo kuwashirikisha waumini kukamilisha.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...