Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Saturday, July 13, 2013

WATU 677 KUSHTAKIWA KWA KUTUMIA VYETI FEKI 677 KUOMBEA KAZI SERIKALINI.

http://www.veta.go.tz/vetanorthernzone/images/veta-logo.jpg OFISI ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imekamata jumla ya vyeti vya kughushi 677 ambavyo wahusika wanadai kuvipata kutoka Wakala wa Usajili, Vizazi na Vifo (RITA), Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA).
Vyeti hivyo vimepelekwa katika taasisi hizo ili kujiridhisha kabla ya kushitaki wahusika kutokana na ofisi hiyo kutokuwa na mamlaka ya kushitaki wenye vyeti ambao hawakupata nafasi hizo.
Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Msemaji wa Ofisi hiyo, Riziki Abrahamu ambaye aliongeza kuwa tangu kuanza kazi kwa Sekretarieti ya Ajira, wameend
esha mchakato wa ajira kwa waombaji 4,891 na kuwapangia vituo vya kazi. 
Alisema kwa mujibu wa sheria, mtu atakayethibitika kughushi nyaraka hizo atahukumiwa kifungo cha miaka 20 jela au kulipa faini ya Sh milioni moja au adhabu zote mbili kwa pamoja. 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...