STAA wa filamu za Kibongo, Wastara Juma amesema hana haraka ya kuolewa kwani anahitaji mume na si mtu wa kupita.
Akizungumza hivi karibuni,
Wastara alisema kwa sasa yupo huru kutoka na mtu yeyote ampendaye
kutokana na sheria na dini inavyosema ila kwa sasa shughuli za kuigiza
zimembana.
Nahitaji
mume na si mtu wa kupita awe mvumilivu, mchapakazi pia awe na hofu ya
Mungu. Kwa sasa nafanya filamu zangu kama kumuenzi marehemu mume wangu, alisema Wastara.