Amesema,
ili kufikia lengo hilo, jamii ya kimataifa inapaswa kuyalazimisha
makundi ya waasi yasitishe vitendo vya utumiaji mabavu na kukaa katika
meza moja ya mazungumzo na serikali ya Sudan. Balozi na mwakilishi wa
kudumu wa Sudan katika Umoja wa Mataifa amesema, serikali ya Khartoum
inaendelea na juhudi zake za kuyakalisha katika meza moja ya mazungumzo
makundi ya waasi lakini jamii ya kimataifa inapaswa kuisaidia nchi yake
katika hilo. Jimbo la Dafur lililoko magharibi mwa Sudan limekuwa
likikabiliwa na hali ya mchafukoge tangu mwaka 2003.



