Vifo vya
raia vinavyotokana na mashambulio ya anga yakiwemo ya ndege zisizo na
rubani za Marekani vimekuwa chanzo cha misuguano kati ya serikali ya
Afghanistan na vikosi vya majeshi ya kigeni yanayoongozwa na Marekani na
kuzidisha pia chuki dhidi ya Washington nchini Afghanistan. Marekani na
waitifaki wake waliivamia Afghanistan mwaka 2001 ikiwa ni katika sehemu
ya kile kilichotajwa kuwa vita dhidi ya ugaidi. Licha ya kuiondoa
madarakani serikali ya kundi la Taliban, machafuko na umwagaji damu
unaendelea kushuhudiwa nchini Afghanistan tangu wakati huo hadi sasa
pamoja na kuweko maelfu ya askari wa majeshi ya kigeni yanayoongozwa na
Marekani



