Waziri
Mkuu wa Uhispania Mariano Rajoy amepuuza wito unaomtaka kujiuzulu
kutokana na kashfa inayoitikisa serikali yake. Ametupilia mbali
shinikizo kutoka kwa wapinzani wake kisiasa ambao wanamtaka kuachia
ngazi kutokana na tuhuma kuwa alipokea malipo ya siri kupitia chama
chake alipokuwa waziri miaka ya 1990.
Rajoy
amewaambia waandishi wa habari mjini Madrid kuwa atakamilisha majukumu
aliyopewa na wapiga kura, na ataendeleza mapambano kujaribu kurejesha
utengamano wa kiuchumi katika nchi yake inayokabiliwa na mdororo.
Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 58 amesema hakufanya kosa lolote.
Mweka
hazina wa chama chake Luis Barcenas ambaye yuko jela kwa hatia ya
kupokea rushwa alitoa ushahidi mahakamani akimshutumu Rajoy na maafisa
wengine wa chama chake kupokea malipo yasio halali. Chama cha Rajoy,
Popular Party kimekanusha kuwepo kwa malipo ya kichinichini.