Amefanya
mazungumzo na rais wa mpito Adly Mansour, waziri mkuu mteule Hazem
el-Beblawi, na kamanda mkuu wa majeshi Jenerali Abdel-Fattah el Sisi.
Maszungumzo hayo yalituama juu ya mpango mpya wa kidemokrasia
uliopendekezwa na uongozi wa sasa.
Mpango
huo unataka katiba iliyoandikwa na vyama vya kiislamu chini ya utawala
wa Morsi ifanyiwe mabadiliko, na kisha uchaguzi wa bunge na rais
ufanyike mapema mwaka kesho. Hadi sasa udugu wa kiislamu umekataa
katakata kushiriki katika mchakato wa sasa wa kisiasa, ukisema hautaki
kuhalalisha mapinduzi yaliyomng'oa Morsi madarakani.