Gazeti
la Wall Street Journal la Marekani limefichua kwamba mpango wa kuiondoa
madarakani serikali ya aliyekuwa rais wa Misri, Muhammad Mursi
ulitayarishwa miezi kadhaa iliyopita kati ya makamanda wa jeshi la nchi
hiyo na vinara wa kambi ya upinzani. Ripoti ya gazeti hilo imeashiria
vikao vya mara kwa mara vya jeshi la Misri na vinara wa kambi ya
upinzani na kwamba jeshi liliwahakikishia wapinzani kwamba, litaingilia
kati kumuondoa madarakani Muhammad Mursi iwapo wapinzani wa serikali
watafanikiwa kukusanya idadi kubwa ya wananchi mitaani.
Gazeti
la Wall Street Journal limefichua kwamba, miongoni mwa waliokuwa
wakihudhuria vikao hivyo ni pamoja na Muhammad el Baradei, Amru Mussa na
Hamdin Sabahi. Limesema kuwa katika vikao hivyo kambi ya upinzani
ilitaka kuhakikishiwa kwamba, jeshi litaingilia kati kumuondoa
madarakani Mursi au la.
Maelfu
ya wananchi wa Misri wanaendelea kufanya maandamano katika miji
mbalimbali ya nchi hiyo wakipinga hatua ya jeshi la nchi hiyo ya
kumuondoa madarakani rais aliyekuwa amechagulwia na wananchi Muhammad
Mursi mapema mwezi huu.