Waandamanaji nchini Misri wakikabiliana kwenye daraja la October usiku wa kuamkia leo.
European Pressphoto Agency
Na Emmanuel Richard Makundi
Maelfu ya
wafuasi wa rais aliyeondolewa madarakani nchini Misri, Mohamed Morsi,
wamekabiliana na polisi kwenye miji mbalimbali nchini humo, safari hii
wakishinikiza kiongozi wao aachiwe huru.
Maandamano
hayo yanafanyika wakati huu ambapo mjumbe wa Marekani kwa nchi ya
Misri, Bill Burns yuko nchini humo kwa mkutano na viongozi wa Serikali
ya mpito kuangalia namna ya kumaliza mzozo wa kisiasa nchini Misri.
Punde
baada ya kuwasili, Burns alitoa wito kwa waziri mkuu Hazem al-Beblawi na
mkuu wa majeshi Abdel Fattah al-Sisi kuhakikisha jeshi halijihusishi na
siasa wala kuwakamata viongozi wa vyama vya siasa kwa shinikizo la
kisiasa.
Burns
ametoa wito huo kufuatia kuendelea kushikiliwa kwa viongozi wengi wa
chama cha Muslim Brotherhood ambapo ameiomba Serikali kuwaachilia huru
viongozi hao akiwemo rais aliyeoondolewa madarakani, Mohamed Morsi.
Marekani
inaonekana kutotaka kujihusisha moja kwa moja na mzozo wa Misri ingawa
iko mstari wa mbele katika kutaka kitafuta suluhu ya kisiasa nchini
humo.
Usiku
kucha waandamanaji wamekabiliana na polisi ambao walilazimika kutumia
mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa Morsi ambao walikuwa
wamezungunga makao makuu ya jeshi.
Licha ya
juhudi ambazo zimeendelea kufanywa na jeshi la nchi hiyo kutaka kuelata
maridhiano, chama cha Muslim Brotherhood kimekataa kujihusisha na
Serikali ya mpito kwa kile viongozi wake wanadai wanamtambua Mohamed
Morsi kama kiongozi wao.
Via kiswahili.rfi.fr