Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Friday, July 12, 2013

Hatimaye Chris Brown akubali matokeo, kwa kuufuta mchoro wa kutisha katika uzio wa nyumba yake!

Breezy graffiti-2

Mwanzoni mwa drama hii Chris Brown alionekana kusimamia misimamo yake, pale alipoamrishwa na vyombo vinavyohusika kuifuta Graffiti aliyoichora katika uzio wa nyumba yake ya Hollywood Hills, Los Angeles, Marekani baada ya majirani na wapita njia kulalamika kuwa unawatisha watoto wao wanaopita katika njia hiyo.
Neighbors complain! Chris Brown paints graffiti on his house
Baada ya malalamiko hayo kuzifikia mamlaka zinazohusika za jiji la Los Angeles, Brown aliamrishwa aufute mchoro huo kitu ambacho alikipinga kwa madai kuwa sheria zinamlinda. Baada ya mvutano wa tokea (May) kati yake na mamlaka ya jiji hilo hatimaye leo (July 12) wafanyakazi wameonekana wakiupaka rangi ukuta huo na kufunika mchoro huo.

Vyanzo vimeuambia mtandao wa TMZ kuwa uamuzi wa kufuta Graffiti hiyo ni wa Chris mwenyewe na sio amri ya jiji la Los Angeles.
Idara ya ujenzi ya Los Angeles imesema endapo mpaka kufikia kesho wataridhishwa kuwa mchoro huo umefutika kabisa, wataifuta fain ambayo ilikuwa apigwe Breezy kwa kuweka mchoro bila kupata vibali.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...