Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Wednesday, June 12, 2013

Msako wa Jeshi la Polisi kanda maalum Dar wafanikisha kukusanya faini ya zaidi ya milioni 64 na kukamata majambazi wanane hatari.

IMG_3013
 Na.Mo Blog Team
 Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeendelea na operesheni mbalimbali kwa mafanikio, ikiwemo kukama wahalifu, kuokoa mali zilzoibiwa na kuwadhibiti madereva wanaokiuka sheria za barabara.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Kamishna wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam Suleiman Kova (pichani) amesema jeshi hilo limefanikiwa kuwakamata majambazi wanane hatari wanaojihusisha na uporaji wa mali za raia wa kigeni ufukweni mwa bahari ya Hindi (Coco Beach).
Pia Kamanda Kova amesema Jeshi hilo limemkamata mtunza bustani aitwaye Philemon Laiza mwenye umri wa miaka 27 mkazi wa Mikocheni B maeneo ya nyumba za serikali anayefanya kazi nyumbani kwa Jaji Kileo, akituhumiwa kuhusika na mauaji ya Perpetua mainab (30) mtumishi wa ndani raia wa Kenya aliyekutwa amekufa baada ya mwili wake kuchinjwa sehemu ya shingo, jeraha mkono wa kushoto karibu na kiganja na jeraha kwenye paji la uso.
Katika tukio lingine, Jeshi hilo limefanikisha kuokolewa kwa mali ya Wachina (Power Tiller) zenye thamani ya Tsh. 157,000,000/= ikiwa ni pamoja na kumkamata tapeli hatari Satara Emmanuel (42)  aliyeitapeli kampuni ya AFRICATIC iliyopo Nyerere Road kwa kuonyesha nyaraka za kugushi kwamba ameshinda zabuni ya ununuzi wa Power Tiller katika Halmashauri ya Mbulu hali akijua anadanganya.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...