Lejendari
 wa soka raia wa Brazil, Pele, anaamini kuwa kurejea kwa kocha mwenye 
maneno mengi, The spesho Jose Mourinho katika klabu yake ya zamani ya 
Chelsea ya jijini London ni chagua sahihi kwa klabu hiyo.
Mashabiki
 wengi wa klabu ya Chelsea wanaamini kuwa kurejea kwa Mourinho darajani,
 mataji ya ligi kuu yatarejea tena klabuni hapo kama miaka ya 2005 na 
2006.
Ingawa
 Pele anakubaki maamuzi ya Roman Abramovich kumrejesha Mourinho, lakini 
ameonya kuwa kurejea kwa kocha huyo sio sababu ya kutegemea mafanikio 
makubwa.
 Pele mwenye umri wa miaka 72, ameimbia televisheni ya CNN  kuwa kurejea kwa Mourinho katika klabu ya Chelsea ni jambo zuri kwani ni kocha bora.
“Ni 
kocha mwenye kipaji kikubwa na mkweli. Najua sana. Lakini soka lina 
maajabu yake. Ana bahati sana katika kazi yake, wakati mwingine kizuri 
huwa hakifanikiwi”. Alisema Pele.
Amerudi mjini: Pele amesema Chelsea imefanya maamuzi sahihi kumrejesha Mourinho darajani
Pele Mpya: Nyota wa Barcelona  Neymar, mwenye umri wa miaka 21, amewavutiwa wengi na kutajwa kuwa Pele mpya wa Brazil.
Wiki hii 
pia habari kubwa wiki hii ni  Neymar kutimka katika klabu ya Santos ya 
Brazil, klabu ambayo Pele alicheza na kuifungia mabao 589 katika michezo
 605 kuanzia mwaka 1956-1974.
Neymar
 ameifungia Santos mabao 54 katika mechi 103 na sasa anatajwa kuwa Pele 
mpya wa Brazil, lakini kwa upnde wake Pele anakataa kumfananisha na 
kinda huyo wa dunia.
Pele
 amekataa kulinganishwa na bwana mdogo Neymar, lakini amekiri kuwa 
kijana huyo ni moja kati ya wachezaji bora zaidi kuwahi kutokea nchini 
Brazil
Pele alisema ” Neymar kuwa kama Pele mpya ni jambo gumu sana kwa sababu mama yangu na baba yangu walishamaliza kazi ya kuzaa”.
 Pele aliendelea kueleza kuwa hakuna shaka kabisa kuwa Neymar ni moja kati ya vipaji vikubwa nchini Brazil.
“Kiukweli
 Brazil vipaji vingi vimewahi kutokea kama Zico, Tostao, Rivelino, Pele,
 Ronaldinho, lakini kwa miaka miwili iliyopita, Neymar ana kipaji 
kikubwa zaidi”. Alisema Pele.



