Nigeria
ni nchi ambayo inafanya vizuri kwenye upande wa entertainment Africa,
lakini kuna wasanii maarufu ambao wanafanya vizuri kwenye burudani huko
Ulaya na Marekani asili yao ni Nigeria. Hawa hapa ni mastaa saba ambao
ni wanaigeria lakini wanafanya vizuri kwenye movie na muziki kwenye
mabala ya Ulaya na Marekani.
JACOB TAIWO CRUZ – TAIWO CRUZ
Taiwo Cruz ni mwimbaji anayefanya kazi zake Ulaya hasa
nchini Uingereza, huyu jamaa kazaliwa kwa baba mwenye asili ya Nigeria
kabisa na mama mwenye asili ya Brazil. Taiwo Cruz alianza kuimba akiwa
na miaka 12 na katika career yake ya muziki ameweza kushinda tuzo kadhaa
kama BRIT awards,ASCAP awards,American Music Awards,Billiboards music
awards na nyingine nyingi. Hata jina lake la Taiwo lina asili ya
Kiyoruba na mara nyingi hupewa kwa mtoto wa kwanza kuzaliwa kama
wamezaliwa mapacha.
LEMAR OBIKA - LEMAR
Lemar alizaliwa Tottenham kwa baba na mama wanigeria
kutoka Enungu kusini mwa Nigeria, Lemar anajulikana kwa kazi yake ya
usanii kwa uimbaji mahiri wa RnB,mwandishi wa nyimbo na producer.
Mashabiki wengi wa msanii huyu hasa wanaigeria, hawakufahamu
kamaLemar ana asili ya Nigeria.
HUGO WEAVING
Actor aliye-act kama agent Smith kwenye movie ya
Matrix ni mnigeria.Jamaa huyu alizaliwa UCH(Univeristy College Hospital
in Ibadan). Hugo akiwa na miezi 12 wazazi wake walihama Nigeria na
kuhamia nchi nyingine.Hivi sasa mnigeria huyu anafanya vizuri huko
Hollywood.
RICHARD AYOADE
Ayoade kazaliwa na baba mnigeria na mama
mnorway.Richard ni comedian maarufu huko Ulaya na mwaka jana alipata
nafasi ya kuigiza kwenye movie ya Hollywood inayoitwa The Watch.Jina
lake la mwisho Ayoade ni jina maarufu sana kwenye kabila la Yoruba
DONALD FAISON
Muigizaji huyu ni maarufu sana huko Hollywood,amezaliwa na baba kutoka nigeria na mama mwenye asili ya kimarekani.
DYLAN KWEBANA MILLSYAnaitwa Dizzle Rascal Dizzie (Dylan Kwebana Mills) ni moja ya marapper wanaopewa heshima sana huko Ulaya. Dizzle aliwahi kushinda tuzo ya BET Act mwaka 2010 na pia alifanya perfomance kwenye sherehe za ufunguzi wa Olympics huko London.
TYLER OKNMA – TYLER THE CREATOR
Huyu jamaa ni maarufu kama “The Black Eminem”. Japokuwa
anasema kwamba hajawahi kukutana na baba yake,Tyler ana asili ya
Nigeria kwasababu baba yake alikuwa mnigeria wa Igbo. The Black
Eminem ambaye ni kiongozi wa kundi la “Odd Future Wolf Kill Them All”,
amewahi kutoa album kadhaa lakini “Bastard” ndiyo album yake maarufu
yenye mistari ya utata kupita kiasi ndio maana akaitwa Black Eminem.



