
Maisha ya wakazi wa
mijini na majijini na maeneo mengine yanayokuwa na hata vijijini yapo
hatarini kiafya, kutokana na kutumia vinywaji vinavyohifadhiwa kwenye
chupa hususan za plasiti zilizotumika.
Chupa hizo ni zile zilizotumiwa na watu tofauti, kisha kutupwa ambapo
zinaokotwa na kuuzwa kwa wahitaji wanaozitumia kuhifadhia vinywaji vya
aina tofauti.
Kutokana na mazingira hayo, watu wengi wapo kwenye hatari ya kuambukizwa
magonjwa ya milipuko kama kuharisha, kipindupindu na kifua kikuu.
Uchunguzi uliofanywa na wataalamu wa afya ya
Mazingira,
umebaini kuwa baadhi ya wafanyabiashara wa vinywaji kama
maji baridi, juisi za aina tofauti, wanatumia chupa zilizotumika,
kuhifadhi vinywaji hivyo.
Hata hivyo, hali hiyo ipo zaidi kwa wafanyabiashara katika maeneo
yanayokaliwa na watu wenye hali duni kiuchumi, hivyo mahitaji ya
vinywaji hivyo vinavyouzwa kwa bei ndogo kuwa makubwa.
Maeneo ambayo yamebainika kuwa na wateja wengi wa bidhaa hizo kuwa ni
shule za msingi na sekondari, sokoni, maeneo ya viwanda, vituo vya
daladala na kwenye makazi duni.

Afisa Afya wa Manispaa ya Temeke jijini Dar es salaam,
anasema chupa hizo ni chafu na hazifai kwa matumizi yaliyozoeleka kwa
baadhi ya wananchi.
Anasema tatizo la watu kuuza vinywaji vinavyohifadhiwa kwenye chupa hizo, limekuwa sugu majiji na maeneo mengine ya nchi.
Anasema matumizi hayo si sahihi kwa vile, chupa hizo si salama na kwamba
watu wanaweza kupata magonjwa ya tumbo, kuharisha na kipindupindu.
Anasema pia endapo mtu aliyetumia chupa hizo ana ugonjwa wa kifua
kikuu, ni rahisi kwa mtu anayeitumia kwa mara ya pili kuathirika kwa
ugonjwa huo.
Watalaam wa afya ya mazingira anasema kitendo cha watu
kuokota chupa zilizotumika na kuhifadhi bidhaa zao, kinapaswa kupigwa
vita ili kunusuru maisha ya watu.
Afisa Afya wa Manispaa ya Temeke anasema ameshashuhudia watu
`wanavyovamia’ maeneo ya viwanja vya soka vya Taifa na Uhuru baada ya
mechi za mpira wa miguu kumalizika, wakiokota chupa zilizotumika.
Anasema mara nyingi mashabiki wengi wanakosa ustaarabu, kiasi cha
kutumia chupa za maji kuhifadhi haja ndogo, jambo linalochangia
kuhalalisha kuwa chupa hizo hazipo salama.
"Mimi naingia mara nyingi kwenye viwanja vile kuangalia mpira, baada ya
mechi, chupa nyingi utaziona zina mikojo na watu wanaziokota, bila shaka
ni miongoni mwa zinazotumika kuhifadhia vinywaji kwa mara ya pili,”
anasema.
Hata hivyo, Inathibitisha kuwepo kwa hali hiyo, na kufafanua kwamba
chupa `zinazozalishwa’ na mashabiki wa mpira, ni kero dhidi ya usafi wa
mazingira katika eneo hilo na hata katika maeneo mengine yenye
mkusanyiko mkubwa wa watu.
WANAFUNZI HATARINI
Katika uchunguzi wa wataalamu wa sayansi ya afya ya mazingira,
imebainika kada iliyo katika hatari zaidi ya kuathirika
kutokana na matumizi ya chupa hizo ni wanafunzi wa shule za msingi na
sekondari.
Katika baadhi ya shule zilizotembelewa katika maeneo tofauti ya mijini na vijijini,
wanafunzi walionekana wakinunua kwa
wingi juisi hizo na kunywa bila kujali kama usafi wake.
Baadhi ya shule zilizoonekana kushamiri kwa biashara.
Walimu wanasema tatizo hilo limekuwa kubwa, likichochewa na wafanyabiashara wanaowalenga wanafunzi kuwa soko la bidhaa zao.
Walimu wanasema baada ya kutoa waraka maalum wa kuzuia biashara hiyo,
wengi wa wafanyabiashara wanauzia nyumbani, hivyo ni vigumu kuwafuata na
kuwazuia.
Mwalimu wa Afya wa Shule ya moja Msingi niliemuuliza anasema shule yake
pamoja na kupiga marufuku biashara hizo, bado watu wanaingiza kinyemela
na kuwauzia wanafunzi.
"Hivi karibuni tumekaa na wafanyabiashara tuliawaambia hatutaki bidhaa
zinazohifadhiwa kwenye chupa au vifaa vilivyotumika, wengi wamekubali
lakini wapo wanaokaidi," anasema Mwalimu huyo.
WAFANYABIASHARA WAJITETEA
Baadhi ya wafanyabiashara wanaouza juisi ya miwa na ya matunda mengine
kwa kutumia chupa zilozotumika, wamesema hawahatarishi afya za
binadamu kwa sababu wanazisafisha kwa kufuata kanuni ya afya.
Wanasema wengi wao wanajua umuhimu wa afya na ndio maana wanapopata chupa hizo, wanazisafisha kwa maji ya moto pamoja na sabuni.
Mmoja wa wafanyabiashara hao, anasema awali alihifadhi juisi
aliyoitengeneza kwenye mifuko maalum ya plastiki, lakini alikuwa
akipungukiwa na wateja kutokana na ugumu wa utumiaji wake.
"Chupa za maji ni nzuri sana hata wateja wetu, wanazipenda na ndio maana
wengi tumeacha kuuza kwenye mifuko ya plastiki," anasema.
Mfanyabiashara mwingine, anasema baadhi yao wameshindwa kufuata kanuni
za afya, hivyo kuwasababishia wengi wao kujikuta wakiingia kwenye kashfa
ya bidhaa chafu.
Nakushauri wewe mtumiaji au Mpenzi wa
Kutumia vinywaji vilivyowekwa kwenye
Chupa ambazo zimekishwa tumika achana nazo kwa ajiri ya afya yako si salama hata kidogo.
Unaweza onani za bei rahisi tu lakini madhara yake ni
makubwa ambayo yanaweza kukugharimu maisha yako pale magonjwa yatakapo
kupata.
Wazazi na walezi wenye watoto wanaoenda shule, ni vyema
mkawashauri kwa kuwaelimisha athari za bidhaa hizo ni vyema kuwapatia
kama ni jiusi au vinywaji vingine toka nyumbani ambayo watatumia wakiwa
maeneo ya shule. chanzo. ManyandaHealthy