Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akizungumza katika
Mkutano wa Teknolojia ya Kupambana na Uhalifu uliofanyika katika Jiji la
Lyon nchini Ufaransa hivi karibuni. Waziri Nchimbi alishiriki mkutano
huo pamoja na washiriki wengine kutoka nchi mbalimbali duniani.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (katikati) akimsikiliza
kwa makini Rais wa Shirika la Kimataifa la Polisi (Interpol), Mireille
Ballestrazzi (kushoto) baada ya Mkutano wa Kimataifa wa Teknolojia ya
Kupambana na Uhalifu uliofanyika katika Jiji la Lyon nchini Ufaransa
hivi karibuni. Kulia ni Meya wa jiji hilo, Gerald Collomb.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (katikati) akiwa katika
picha ya pamoja na Rais wa Shirika la Kimataifa la Polisi (Interpol)
Mireille Ballestrazzi (kushoto) na Kulia ni Meya wa Jiji la Lyon, Gerald
Collomb. Waziri Nchimbi alishiriki mkutano huo wa Kimataifa hivi
karibuni. Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi.