Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Friday, July 12, 2013

WAKULIMA WA MBOGA MBOGA WATAKIWA KUTUMIA FURSA KUPITIA TAHA


agricultural_produce

Na  Khadija khamis –Maelezo Zanzibar 
NAIBU wazri wa kilimo na mali ya asili  Mtumwa Kheri Mbarouk amewataka wakulima wa mboga mboga na matunda kuitumia fursa wanayoipata kupitia taasisi ya kusaidia wakulima wa mboga mboga na matunda Tanzania (TAHA) katika kukiimarisha kilimo hicho.

Aliyaeleza hayo jana waziri huyo katika uzinduzi wa ofisi na miradi ya TAHA Zanzibar iliyofanyika katika ofisi ya mfuko wa barabara Kikwajuni mjini Zanzibar.

Alisema ipo haja kwa wakulima hao kuimarisha kilimo hicho, kukitunza  na kuithamini ili iwe mkombozi katika kuleta mapinduzi ya kilimo.

“Mafanikio tuliyoyapata yameleta tija na bado tunahitaji kilimo bora na chenye manufaa katika kukuza sekta ya kilimo katika nchi yetu .” Alisema Naibu waziri Mtumwa
Aidha alisema changamoto iliyopo hivi sasa ni ukosefu mkubwa wa soko,  hivyo serikali iko mbioni kulitafutia ufumbuzi tatizo hilo.

Alisema, iwapo kilimo hicho kitaimarika na kuweza kumnufaisha mtumiaji na mlaji na kutaweza kupatikana matumaini makubwa kwa kupata kuzalishwa kwa mbegu ziliobora kwa wakulima waliowengi.

Pia aliwataka wakulima hao wasivunjike  moyo wala wasiwe na wasiwasi na badala yake wakaze mkanda  nayo serikali na taasisi hiyo ya TAHA itajitahidi kuwatafutia ufumbuzi wa soko la ndani na lanje ili kuweza kuimarisha zaidi kilimo cha kisasa.

Nae Mkurugenzi wa TAHA Jaclin Nkinda wakati akitoa nasaha kwa wakulima alisema kilimo bila ya wanawake haiwezekani kwani wanawake ni wakulima wakubwa katika kilomo cha mboga mboga na matunda hapa kwetu Zanzibar. 

Jaclin alisema Taasisis ya TAHA ina lengo la kuwasaidia wakulima wa mboga mboga na matunda kwa nia ya uzalishaji wa mbegu Tanzania bara ili kuleta na kuendeleza kilimo hicho hapo baadae.

Sambamba na wafadhili,Mfadhili kutoka Finland Tina Huvis alisema Zanzibar inazalisha mboga mboga nyingi ambayo ina lengo la kuisaidi serikali na wakulima wa Unguja ili kufanikisha kilimo cha mboga mboga.

Alisema wafadhili hao wataendeleza mashirikiano yao ili kuleta maendeleo ya kilimo hicho.

Jumuiya hiyo ilianzishwa mwaka 2004 yenye lengo la kuimarisha kilimo hapa nchini ikiwa na wadgamini wawili kutoka Filand na USAID

  IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...