WASHIRIKI waliokuwa wakiwakilisha Shindano la Vigori 2013 linaloendeshwa na mtangazaji maarufu Bongo, Maimartha Jesse, Stella Manyanya na Anita James wamemkimbia bosi wao huyo baada ya kuona hakuna kinachoendelea.
‘Tumeamua kumkimbia Maimartha sababu tulikuwa tukisubiri simu kila siku tunaona mambo hayaeleweki ndipo tukaamua kujiunga na Classic Girls chini yake Monalisa Ivan,’’ alisema Stella.