Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Tuesday, July 2, 2013

TUNAOMBA RADHI KWA PICHA HIZI:AJALI MBAYA YATOKEA MAENEO YA MABIBO EXTERNAL

Kama ule usemi usemao hatujui yatakayo tokea kesho, ndicho kilichotokea majira ya saa moja jana jioni  tarehe 02/07/2013, baada ya gari dogo lililokuwa linatokea maeneo ya Ubungo kwenda uelekeo wa Buguruni kumgonga mwenda kwa miguu aliyekuwa anavuka barabara katika maeneo Gereji (garage) Maeneo haya ni mara baada ya kituo cha daladala Mabibo External, kituo kinachofuata kama unakwenda Buguruni kinaitwa Gereji, hapa ndipo ilipotokea ajali hiyo  mtu aliyegongwa hakuweza kufahamika kwa wakati huo na mashuhuda wengi wa ajali hiyo, lakini ni kijana wa kiume mwenye umri kati ya miaka 30 na 22, rangi yake ni mweusi,  na alikuwa amevaa t-shirt nyeupe iliyokuwa na maandishi ya ADIDAS,
Kwa hakika maisha yetu wanadamu ni mafupi sana!! tunaweza kuwa na mipango mengi na malengo mazuri sana, lakini mwisho wetu ukawa hivi pasipo hata kutarajia!! ndio maana wale wanao amini juu ya maisha mengine baada ya kifo, wanfundisha na kusema tunapaswa kujiweka tayari kiroho wakati wote
Endelea kusoma habari hii kwa kubofya hapa chini


Damu iliyotoka ni nyingi sana
Damu ilimtoka kwa wingi sana mara baada ya ajali katika maeneo ya kichwani, na hapo ilipotokea ajali kuna kivuko cha waendeo kwa miguu!! kwa mtazamo usio na uthibitisho wa daktari, kijana huyo alifariki muda mfupi baada ya ajali. Tunaomba kuchukua nafasi hii kuwakumbusha madereva wote wazingatie sheria za usalama barabarani, hapa ilipotokea ajali kuna kivuko cha waenda kwa miguu na pia kuna kituo cha mabasi (daladala) kwa vyovyote dereva alitakiwa kupungumza mwendo na hata kama pa mtu anavuka angeweza kumwona na kuepusha ajali. Tunaliomba jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani, wasichoke kuwaelimisha madereva juu ya alama za barabarani.
Source:  Darubini Leo
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...