Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Tuesday, July 2, 2013

Odama wa bongo movies afuata nyayo za Vicent kigosi (Ray)



Katika kile kinachoonekana ni mpango mkakati wa waigizaji wa bongomovies kujiweka vizuri zaidi kiafya kutokana na ‘’bata’’ nyingi wanazokula, mwigizaji mwingine wa tasnia hii Jennifer Kyaka ama Odama, naye ameamua kuingia gym kwa ajili ya kuuweka mwili wake safi zaidi. Katika picha alizoweka mtandaoni hivi karibuni zilimuonesha mwanadada huyu akiwa maeneo hayo ya mazoezi na aliandika:

‘’Hizi ndio harakati za kuweka mwili sawa,Moja ya vitu muhimu katika maisha ya mwanadamu ni kuhakikisha anafanya mazoezi ili mwili uwe na afya nzuri so huwa napenda kufanya mazoezi kama hivi...........’’ Kwenye picha hizo

Hii inakuja baada ya msanii mwingine Vicent Kigosi (Ray) kuamua kuingia kwenye mchakato wa mazoezi makali sana kupunguza mwili wake ambao wadau wengi wa bongomovies walisema kuwa haumpendezi.

Hongera sana dada odama!




Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...