Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Monday, July 15, 2013

OCD MBINGA ALALAMIKIWA NA ASKARI

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhfkCSmK5JEDxXT-L76UkK4wnPRjzd9RTbIAD_1sp4wuydFMo1zh2T2mUkHAASOpGtfE0dvkeoiwhjg2aD546j5rBGgAwQa36B5zJqpcJk5YIoJMYRRTQIjMiVJH06A5DmJCajilYwuf6Y/s1600/Police1.jpg
 

Na Muhidin Amri–Mbinga,


BAADHI ya askari polisi wa kituo kikuu  Mbinga mjini,wamemtuhumu mkuu wa polisi wa wilaya hiyo(OCD)Jastine Joseph kuwa ni mtu anayetumia madaraka yake vibaya kwa kuendesha manyanyaso dhidi ya askari wa vyeo vya chini na kumuomba Mkuu wa jeshi ilo Said Mwema kumuondoa haraka kabla ya hali haijawa mbaya zaidi.

Wakizungumza na mtandao huu  kwa masharti ya kutotajwa majina yao,askari hao wamelalamika kuwa OCD wao amekuwa akitoa lugha za dharau na hata  zisizopendeza kwao hali inayowavunja moyo wa kazi askari wengine katika wilaya hiyo.

Walisema,iwapo jeshi litashindwa kumuhamisha Jastine kunaweza kutokea maafa makubwa kwani hawatoweza kuvumilia vitendo vinavyofanywa na afisa huyo hasa ukizingatia kuwa na wao ni watu wakubwa tena wenye familia kama yeye hivyo kitendo cha kuwatolea lugha za kiuni ni sawa na kuwadhalilisha.

Aidha wameshauri hata maafisa wengine katika wilaya hiyo wanatakiwa kuondoka kwani wameshaaka Mbinga kwa muda mrefu hivyo ni vema kupelekwa katika maeneo mengine ya nchi ili wakapate changamoto mpya za utendaji wa kazi, na kuendelea kuwepo katika wilaya hiyo ni tatizo kubwa kwani wameshafahamika na watu wengine hali inayowafanya kushindwa kuchukua maamuzi sahihi.

Wamesema ocd wao ni mtu hasiyetaka ushauri kutoka kwa mwingine hata kwa maafisa wenzake jambo linalomfanya kutengwa na kujikuta na yuko pekee yake au na wale askari wa kabila lake tu jambo lililowafanya askari kuwepo katika makundi hasa baada ya kufika Jastine kitu ambacho siku za nyuma hakikuwepo na askari wote walikuwa ndugu moja wakiishi na kusaidiana tofauti na sasa.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...