Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Saturday, July 13, 2013

Mjahidina wa Kenya aibuka tena, adhihirisha hali ya sasa ya Al-Shabaab


"Sina cheo [katika al-Shabaab] kwa wakati huu wala sijioni mwenyewe kushika cheo chochote kwa siku zijazo," Mjahidina wa Kenya Ahmad Iman Ali alisema wakati wa mahojiano ya hivi karibuni na Kituo cha Vijana wa Kiislamu cha Kenya. [Jalada]
 
 
 
Na Bosire Boniface, Garissa

Katika mahojiano ya hivi karibuni na Kituo cha Vijana wa Kiislamu cha Kenya (MYC), Mjahidina wa Kenya Ahmad Iman Ali alikana jukumu lake la uongozi ndani ya al-Shabaab na kutoa kauli ya kujisalimisha na utiifu wake kamili kwa kiongozi wa juu wa al-Shabaab Ahmed Abdi Godane.

"[Tu] nahitaji kuelewa kwamba kutoa utiifu wetu kwa kamanda wetu [Godane], wakati tunamsikiliza na kumtii kwa kile ambacho hakikatazwi kunachukuliwa kama ibada ya lazima [tendo la ibada], na ninamshukuru Allah SW [Apewe utukufu na kutukuzwa sana] kwamba ninatimiza majukumu yangu pasipo kulazimishwa na mtu yeyote," alisema katika mahojiano yaliyoshapishwa tarehe 4 Julai kupitia Twitter.

Hii ni mara ya kwanza Ali -- ambaye huko nyuma alitajwa kama "Emiri mkuu wa Kenya wa al-Shabaab" -- amezungumza hadharani kutoka alipoondoka kwenye taifa lake la uraia la Kenya kwenda Kismayu mwaka 2009 pamoja na mamia ya askari wa Kenya.

Wakaazi wa wilaya ya Warta Nabada ya Mogadishu, ambayo ilikuwa ikijulikana kama Wardhigley, walikamatwa wakati wa operesheni ya polisi tarehe 21 Mei kuwaondoa wanachama wa al-Shabaab katika mji mkuu wa Somalia. [Na AFP/AU UN 1st Photo/Tobin Jones]

Kiapo cha utiifu cha Ali kimekuja wakati Godane akiwa anapigana na uasi wa wazi kutoka kwa idadi kadhaa ya viongozi waandamizi wa al-Shabaab wanaompinga kwa kile wanachokiita utawala wake dhalimu.


Hata hivyo, sharti la Ali la utiifu "wa kile kisichokatazwa" halina uzito kwa sababu maulamaa na wanazuoni wa Kiislamu walikosoa uhalali wa tafsiri ya dini ya Godane. Matumizi ya Godane ya misemo ya Nabii Mohammed na mistari ya Qu'ran nje ya muktadha kuhalalisha mauaji ya wanaompinga ni kuharibu Uislamu, Kiiongozi wa dini wa Somalia aliiambia Sabahi, kwa hiyo wafuasi wa Godane hawalazimishwi kumtii kiongozi wa al-Shabaab katika vitendo vya dhambi.

Akiuliza iwapo jihadi inapaswa kuwa ya kidunia au katika mawanda ya eneo -- suala lililo la kimkakati ambalo limekuwa suala lenye utata miongoni mwa viongozi wa al-Shabaab -- Ali alionekana kuwa sambamba na Godane. "Jihad ni ya aina mbili : mashambulizi na kujilinda, na kujilinda kunapewa kipaumbele," alisema.

Akiri uasi mkubwa, akana jukumu la uongozi katika al-Shabaab
Ali alikiri kuongezeka kwa kiwango cha waasi, lakini alikana tuhuma kwamba aliwaacha askari vijana wakiwa wamekwama katika uwanja wa mapigano.

"Sijasikia yeyote aliyekimbia kwenye uwanja wa mapambano na kutumia jina langu kama kisingizio, kama walikuwepo huko nina wapongeza kwa unyofu wao," alisema. "[Mimi] siko katika nafasi ya kutoa uhakikisho."

Ali alikiri kulikuwepo na idadi kadhaa ya askari wa Kenya "ambao walidai kuondoka Somalia kwa sababu sijawasaidia kamwe".

"Safari yangu ya kwenda kwenye jihadi ilikuwa jukumu ambalo niliahirisha kwa muda mrefu na nilikuwa nikiwashauri vijana, kila saa, kwamba jukumu letu liko katika uwanja wa mapambano. Kwa hivyo yeyote anayefikiri kuwamba niliwaondoa kwa sababu ya madaraka na umaarufu, jibu langu ni ndiyo lakini madaraka na umaarufu, [viko] akhera [baada ya maisha], siyo katika dunia hii," alisema.

Ali aliendelea kupinga kwamba hajawahi kuchaguliwa kuwa amiri mkuu wa al-Shabaab Kenya mwezi Januari 2012 -- ambao MYC ilithibitisha kwa wakati huo, akiita "utambuzi kutoka kwa ndugu zetu wa Somalia ambao wamekuwa wakipigana bila kuchoka dhidi ya wasioamini kuhusu umuhimu wa Wajahidina wa Kenya nchini Somalia".

Hata hivyo, Ali alisema hajawahi kusikia tangazo kama hilo. "[Kama] nilivyosema sijawa na cheo, mimi ni Mjahidina [mpiganaji wa jihadi] kama walivyo wajahidina wengine wowote kwa hivyo kunichukulia kama amiri nchini Kenya haina mafanikio wala kushindwa kwani nafasi yenyewe haipo ," alisema. "Kama nilivyosema mwanzo sina cheo kwa sasa na wala sijioni mwenyewe kuwa na cheo kwa siku zijazo."

Uchambuzi wa kufa moyo kwa al-Shabaab
Pamoja na mahojiano kutaka kuwashawishi wafuasi kujiunga na mapigano huko Somalia, Ali bila ya kukusudia alibaini zaidi juu ya mapigano ya nguvu na mienendo ndani ya kikundi kisichoungana na kilichokufa moyo, alisema David Ochami, mwandishi wa habari anayeishi Mombasa ambaye anaandikia gazeti la The Standard la Kenya kuhusu vikosi vya wanamgambo Mashariki ya Kati na Pembe ya Afrika.

"Inaonyesha mahojiano yalipangwa na kusimamiwa na al-Shabaab kuonyesha kwamba wapiganaji wameungana chini ya kiongozi wa al-Shabaab Ahmed Abdi Godane," aliiambia Sabahi. "Kwa kuahidi utii kwa Godane, al-Shabaab inatuma ujumbe huo kwa wapiganaji wanaoasi na wanaoukosoa uongozi wa Godane kubadilisha mawazo yao na kurejea katika kundi hicho."

Alionyesha katika majibizano ya ujumbe wa moja kwa moja kati ya MYC na al-Shabaab katika Twitter siku mbili kabla ya mahojiano kuchapishwa kama ushahidi ambao labda ulifanyika na al- Shabaab huko Somalia na kutumwa kwa MYC kutangazwa.

Kwa kufuta nafasi ya Ali miezi 18 baada ya kutajwa, al-Shabaab iko wazi mno kumuonyesha Godane kama nguvu pekee ya kati, alisema Ochami.

"Katika umma, Ali anajifanya kama kibaraka kwa kukubali kuonekana mbaya, lakini ushushaji wa cheo ungeweza pia kufanya kutoridhika zaidi miongoni mwa wafuasi wake ambao wanamuona kama kiongozi," alisema.

Kupotosha yaliyopita, kuwabughudhi raia
Katika mahojiano, Ali alijaribu kuchochea hisia za kisasi kwa kulinganisha mapigano ya wanamgambo wa al-Shabaab wa Kenya na majanga yasiyohusiana ya miongo iliyopita.

"Eneo la vita bado halijapitiwa kwa matangazo ila kwa uadui unaoonyeshwa na makafiri [makafiri] hata kama hakuna anayefanya matangazo yoyote yanayohusika," alisema. "Kwa hiyo Kenya lilikuwa ni eneo la vita tangu wakati wa mauaji ya Wagalla."

Tukio la mwaka 1984 lilikuwa ni matokeo ya mapigano ya muda mrefu kuhusu ardhi kati ya koo za Kiislamu za Degodia na Ajuran. Katika tukio hilo, maofisa waliopelekwa kurejesha amri waliwaua maelfu ya watu, ambayo serikali ya Kenya ilikiri mwaka 2000.

Katika ripoti iliyowasilishwa kwa Rais Uhuru Kenyatta tarehe 21 May, Tume ya Haki ya Kweli na Maridhiano iliorodhesha aina za uvunjaji wa haki za binadamu kutokana na tukio la Wagalla na matukio mengine, na kutoa mapendekezo kuzuia kujirudia kwa historia. Ripoti itawasilishwa katika bunge kwa ajili ya majadiliano katika tarehe ambayo bado haijapangwa.

Kurejelea mauaji ya Wagalla ni jaribio rahisi ya kushawishi raia kwa kuchochea hisia miongoni mwa wakaazi wa Wajir wanaopenda amani, alisema Kamishna wa Kaunti ya Wajir Naftali Mung'athia.

Hadi wakati wa mahojiano, MYC ilithibitisha shughuli zake za kijihadi kuhusu ushiriki wa Kenya katika Misheni ya Afrika ya Mashariki nchini Somalia na urejeshaji wa serikali ya Somalia. Hata hivyo, katika mahojiano haya, kikundi kilirekebisha nafasi yake na kutumia migogoro ya koo nchini Kenya kuwavutia wapiganaji wapya, alisema Mung'athia.

Mahojiano yasiyokuwa ya kawaida ya Ali pia ni jaribio la kutengua uharibifu uliosababishwa na mwanajihadi aliyezaliwa Marekani Abu Mansoor al-Amriki, ambaye alielezea kwa undani kuhusu kutoelewana miongoni mwa viongozi wa al-Shabaab kuhusiana na mkakati wa kikundi, alisema.

"[Al-Amriki] alifanya uharibifu mkubwa na kikundi kinajitokeza wakati hayupo tena katika eneo la tukio katika jaribio la kurejesha propaganda zao katika mstari na kuokoa sura," aliiambia Sabahi.

Kumuuliza mtu kama Ali, ambaye kwa msisitizo anakanusha kushikilia nafasi yoyote katika vyeo vya al-Shabaab, kufanya mahojiano kunaashiria ufafanuzi wa Godane ni kwa ajili ya kuungwa mkono, alisema Meja mstaafu wa Jeshi la Ulinzi la Kenya Bashir Hajji Abdullahi.

Godane amekwishiwa na washirika katika jitihada zake za kuwa na mamlaka kamili ya kikundi hicho kilichotengana, lakini mahojiano haya hayataweza kuwashawishi waasi kurejea katika kikundi, alisema.

"Uharibifu ulifanyika kwa alivyofanyiwa [Abu Mansoor al-Amriki] na viongozi wengine wa al-Shabaab," aliiambia Sabahi. "Askari wa miguu wanaangalia usimamizi wa viongozi wao na kuhitimisha kwamba jambo hilo hilo litatokea kwa wa vyeo vya chini."

Chanzo - abahionline.com
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...