Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Saturday, July 13, 2013

KAMATI KUCHUNGUZA BEI ZA VYAKULA MFUNGO WA RAMADHANI

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhuvLS19NOEcetX1KuNetyZHGyH34pQu89ek5KV5AiEBddtocfm-8ho7EvLOMquIxIR4ntCUbLxaXO_sQOvLLGkO6M8zExX-3Y2Af50y7ssjNAoz1i92TaSyoW1coXQzhnjK0YtkDf9LTr-/s1600/IMG_5198.JPG

Kamati ya kuchunguza bei ya vyakula  katika kipindi hiki cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani iliyoudwa na mkuu wa mkoa wa Dodoma  Dr Rehema Chimbi imebaini  kuwa hadi sasa bei ya vyakula haijapanda katika masoko na maeneo mbalimbali mkoani Dodoma.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Alhaji Mussa Kasmir amesema hayo leo wakati akiongea na waandishi wa habari kwenye ukumbi uliopo kwenye ofisi ya  mkuu wa mkoa Dodoma.

Alhaji Kasmiri amesema kuwa kamati hiyo iliyoundwa  kuchunguza bei imemshirikisha afisa biashara mkoa ,Mwenyekiti wa TCCIA mkoa na afisa masoko na.

 Amesema kuwa walitembelea masoko yote na kubaini kuwa hakuna badiliko la bei.

Aidha  Mwenyekiti huyo amesema kuwa kamati imefanya uchunguzi katika maghala ya chakula na amewahamasisha wafanya biashara  kutopandisha bei katika kipindi hiki cha mwezi wa Ramadhani na atakayekiuka atachukuliwa hatua stahiki.

CHANZO: Redio Mwangaza FM, Dodoma-Tanzania

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...