Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Monday, July 15, 2013

JWTZ KUONGEZA WANAJESHI ZAIDI WA KULINDA AMANI DARFUR NCHINI SUDAN.

JWTZ kuongeza nguvu zaidi Darfur 

JESHI la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), linatarajia kuongeza nguvu ya kujilinda, wakati wa kulinda amani katika Jimbo la Darfur nchini Sudan, ili kujikinga na mashambulizi kama la juzi, ambalo lilisababisha askari wake saba kupoteza maisha.
Msemaji wa JWTZ Kanali Kapambala Mgawe, alisema hayo jijini Dar es Salaam jana, wakati akizungumzia shambulio hilo, lililosababisha pia majeruhi wengine 14.

Kauli hiyo imetolewa wakati Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete akiungana na Watanzania wote na hasa maofisa na wapigan
aji wa JWTZ na familia za wafiwa, kuomboleza vifo vya vijana hao hodari wa Tanzania.
Nguvu zaidi

Kanali Mgawe alisema mawasiliano yanafanyika kati JWTZ na Umoja wa Mataifa (UN), kuhusu uwezekano wa kuongeza uwezo wa kujilinda na mashambulizi, wakati askari wa Tanzania wanapokabiliana na mashambulizi hayo.

“Kama inavyojulikana, kikosi chetu kipo kule kulinda amani kwa mujibu wa makubaliano ya Umoja wa Mataifa (UN) Sura ya Sita, ambayo yanataka kusitumike nguvu sana, sasa tunataka tutumie Sura ya Saba inayotoa fursa ya kuongeza uwezo wa kujilinda.
“Mawasiliano yanafanyika kati yetu na UN kuhusu uwezekano wa kuongeza uwezo wa kujilinda na mashambulizi wakati wa mashambulizi hayo,” alisema Kanali Mgawe.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...