Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Friday, July 12, 2013

BAADA YA NDOA YA DIDA ,ATAKIWA ATULIE


BAADA ya hivi karibuni Mtangazaji wa Radio Times, Khadija Shaibu ‘Dida’ kufunga ndoa na mwanaume aitwaye Ezden, Marafiki zake wamemtaka kutulia sasa na asijaribu kugeuza ndoa kuwa fasheni.







































Khadija Shaibu ‘Dida’ na mumewe Ezden

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya mastaa walioomba hifadhi ya majina yao ambao walihudhuria ndoa hiyo iliyofungwa wiki iliyopita Ubungo jijini Dar walisema, wamechoka na mialiko ya ndoa zake kila baada ya kipindi kifupi hivyo ni wakati sasa wa kutulia.









































“Asifanye ndoa kama fasheni, tumechoka kuhudhuria sherehe za ndoa yake, kama ana kasoro, ajirekebishe ili atulie sasa ajenge maisha yake,” alisema staa mmoja ambaye ni rafiki wa karibu na ndugu wa Dida.

Hata hivyo, akizungumzia kuhusu kuolewa huko, Dida alisema safari hii ndoa yake ikivunjika haolewi tena.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...