
Ndugu, marafiki, wasanii, watu mashuhuri na watu wa aina mbalimbali leo wamejumuika kwenye mazishi ya rapper Langa Kileo aliyefariki wiki iliyopita kwenye hospitali ya taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam. Langa amezikwa kwenye makaburi ya Kinondoni ambapo mazishi yake yameongozwa na wazazi wake wote wawili. Hizi ni baadhi ya picha za mazishi hayo.






























