Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Friday, June 21, 2013

MKE WA NAIBU CHIFU AFARIKI DUNIA MARA BAADA YA KUNYWA GONGO KUPITA KIASI...!!


changaa
MKE wa naibu wa chifu katika wilaya ya Marigat Alhamisi aliaga dunia katika hali isioeleweka baada ya mumewe kumpata akinywa pombe haramu ya chang’aa katika nyumba ya jirani.


Naibu wa chifu wa kata ya Arabal Bw William Yegon inasemekana hakufurahia pale alipompata mkewe Bi Mary Kobilo, 46, akipiga mtindi na wanakijiji wengine.



Wenyeji walioongea na Taifa Leo walisema kuwa wawili hao walianza kuzozana wakati wa tukio hilo la saa kumi na mbili jioni Jumatano huku naibu huyo wa chifu akimlaumu mkewe kwa kumwaibisha kwa kunywa pombe hiyo haramu ilhali yeye alikuwa afisa wa serikali anayefaa kuongoza vita dhidi ya pombe haramu.


Naibu huyo wa chifu alikasirishwa sana kwamba mkewe alikuwa akimkosea heshima licha ya serikali kutangaza vita kwa wapikaji wa pombe haramu,”alisema mmoja wa wanakijiji ambao hakutaka kutajwa jina.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...