Maelfu ya
waandamanaji wameandamana katika barabara za mjini Addis Ababa,
Ethiopia, wakidai waandishi wa habari na wanaharakati walioko kizuizini
wafunguliwe.
Waandishi
wa habari wanasema ni nadra kuonesha upinzani wa namna hiyo kwa chama
tawala ambacho kinadhibiti shughuli za jamii sawasawa.
Makundi
ya kutetea haki za kibinaadamu yanasema serikali imetumia sheria za
kupambana na ugaidi ili kuwafunga waandishi wa habari.
Waandamanaji- wengi kutoka upinzani - walipiga kelele kudai uhuru na haki.
Haya ni
maandamano ya kwanza tangu mwaka wa 2005 ambapo mamia ya waandamanaji
waliuliwa katika ghasia zilizofuatia uchaguzi. Chanzo: bbcswahili