Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Friday, June 7, 2013

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, JOHN CASMIR MINJA AWAPANDISHA VYEO

 
ASKARI 984  Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja -- Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja leo amewapandisha Cheo Jumla ya Askari Magereza 984  kuwa Koplo wa Magereza, kati yao wanaume ni 845 na wanawake ni 139 baada ya kuhitimu ya kuhitimu Mafunzo  ya Uongozi katika Chuo cha Magereza Kiwira, Mbeya.  Akifunga Mafunzo ya Uongozi wa Daraja la Kwanza kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Magereza, Kamishna wa Utawala na Fedha wa Jeshi la Magereza, Gaston Sanga amewapongeza wahitimu hao kwa kufanya vizuri katika masomo Yao  na hivyo kustahili kuwa  Viongozi katika ngazi ya kwanza(NCO's) katika Jeshi la Magereza.   Amewaasa kuzingatia kikamilifu weledi katika kutekeleza majukumu yao ya kazi na kuhakikisha Kuwa wanalinda, kutetea pamoja na kusimamia haki za wafungwa kwa  mujibu wa taratibu za Magereza ili kulinda utu wa Wafungwa pamoja na hadhi ya Jeshi la Magereza.  
Wahitimu hao wameshiriki kikamilifu katika Mafunzo ya Nyanja zinazohusu Utawala na Uendeshaji wa Magereza, Ustawi wa Jamii, Uraia, Afya pamoja na Mafunzo ya Kijeshi. Pia kwa kuzingatia madhara ya Adui rushwa, wahitimu hao  wamefundishwa kwa kina juu ya madhara yatokanayo na rushwa, mazingira na vita dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi.   Pia wahitimu hao wa Kozi Namba 20 ya Uongozi daraja la kwanza wamepongezwa na Mgeni rasmi, Kamishna Gaston Sanga kwa mchango wao wa hiari kwa kujitolea Tsh. 2,000,000/= kwa ajili ya kuboresha jiko na miundombinu mingine ya Chuoni hapo.    Imetolewa na; INSP. Lucas Mboje, Afisa Habari wa Jeshi la Magereza.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...