Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Saturday, May 4, 2013

MZEE NGASSA,NA MZEE TEGETE USO KWA USO CCM KIRUMBA


 Kutoka kushoto ni John Tegete baba mzazi wa mchezaji nyota wa yanga Jerry Tegete,kulia ni Kalfan Ngassa baba mzazi wa mchezaji nyota wa Simba Mrisho Ngassa,wakihojiwa na mtandao huu ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza jumamosi iliyopita.Mrisho ni mtoto wa Khalfani Ngassa aliyewahi kung'ara na timu ya Pamba ya Mwanza na Simba huku Mzee Tegete pia aliwa kuwa mchezaji tegemeo wa Pamba wakati watoto zao wakingara kwenye timu kubwa za simba na yanga wazee hao wanaendeleza fani hii ya Soka ambapo mzee Tegete mbali ya kuwa meneja wa uwanja wa CCM Kirumba pia ni kocha mkuu wa timu ya Toto Afrika iliyoshuka daraja msimu huu huku Mzee Ngassa akipewa jukumu la ukocha mkuu timu ya Polisi lringa inayoshiriki ligi daraja la kwanza.


Juzi jumamosi Mtandao huu uliwafuma wazee hao wakibadilishana mawazo huku wakiwa na furaha na afya njema wakiendela kula matunda ya watoto wao ambao mbali ya kuwa tegemo kwa timu zao pia ni wachezaji muhimu kwa timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars.kwa sasa.
Kwa pamoja walipohojiwa na mwandishi wa habari hizi kuhusiana na maendela ya watoto wao wazee hao walidai kwamba kila kukicha wanawaasa watoto zaokufanya mazoezi kwa bidii na kuepukana na mambo ya anafa ambayo.


Kutoka kulini ni Juma Amir,kati John Tegete na kulia ni Khalfani Ngassa wakiwa kwenye picha ya pamoja  baada ya kuhojiwa na matanda huu.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...