Kikosi cha tume ya Umoja wa
Afrika nchini Somalia AMISOM kimesema kimevunja jaribio la mashambulizi
mawili yaliyopangwa kufanywa wiki hii na magaidi wanaodhaniwa kutoka
kundi la Al shabaab dhidi ya bandari ya Kismayu.
Kamanda wa kikosi cha AMOSOM Bw Andrew Gutti ametoa taarifa akisema, majeshi ya AMISOM yalimkamata mwanamke aliyekuwa na mabomu akijaribu kuingia katika Chuo Kikuu cha Kismayu, ambako wajumbe walikuwa wanakutana kujadili mchakato wa kisiasa wa Jubaland.
Majeshi hayo pia yamezuia jaribio lingine la shambulizi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kismayu.
Bw Gutti amesema kundi moja la watu waliokuwa wanapanga kufanya shambulizi kwenye uwanja wa ndege liligunduliwa na wanajeshi wa AMISOM na kupambana nao.
Magaidi hao waliwashambulia wanajeshi wa AMISOM kwa mizinga, baadhi ya mizinga iliangukia karibu na uwanja wa ndege, na magaidi hao walikimbia.
Kamanda wa kikosi cha AMOSOM Bw Andrew Gutti ametoa taarifa akisema, majeshi ya AMISOM yalimkamata mwanamke aliyekuwa na mabomu akijaribu kuingia katika Chuo Kikuu cha Kismayu, ambako wajumbe walikuwa wanakutana kujadili mchakato wa kisiasa wa Jubaland.
Majeshi hayo pia yamezuia jaribio lingine la shambulizi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kismayu.
Bw Gutti amesema kundi moja la watu waliokuwa wanapanga kufanya shambulizi kwenye uwanja wa ndege liligunduliwa na wanajeshi wa AMISOM na kupambana nao.
Magaidi hao waliwashambulia wanajeshi wa AMISOM kwa mizinga, baadhi ya mizinga iliangukia karibu na uwanja wa ndege, na magaidi hao walikimbia.




