Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Wednesday, May 22, 2013

HAYA NDIO MAAJABU YA MSIKITI WA KAOLE,BAGAMOYO

  Kabla ya kuingia magofu hayo ya kale unakutana na tangazo hili
                                                            Sehemu ya Choo
 Mzee Mohamed Pazi [80] ambaye amezaliwa na kukulia kijiji hicho cha Kaole,akiwa nje ya ofisi za makumbusho hayo
 Baada ya muda Mtandao huu ulimshuhudia Mzee Mohamed Pazzi akiingia kwenye Msikiti huo wa kale.
   Akiingia ndani
  Sehemu ya Kibla ya msikiti huo wa kale uliojengwa kalne ya 13
                               Mzee Pazzi akiswari kwenye msikiti huo wa Kale eneo la Kibla
 Pia Mtandao huu uliwashuhudia baadhi ya watalii  wa ndani wakinawa maji ya baraka yaliopo eneo la Msikiti huo kwa lengo la kujisafisha na kweda kuswari kwenye msikiti huo wa kale
  Watalii hao wa ndani wakiswari kwenye Msikitim huo
Sehemu ya msikiti huo ambayo pembeni yake kuna kisima chenye maji ya baraka,
       Sehemu ya Msikiti huo uliojengwa karne ya 13 ikumbukwe hii ni karne ya 21
HAYA ni makumbusho ya Msikiti wa kale uliojengwa karne ya 13 kijiji cha Kaole Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani,ambapo pepezoni ya Msikiti huo kuna kisima chenye maji ya baraka huku ikidaiwa kwamba maji hayo ya baraka hayajawahi kupungua wala kuongezeka toka karne hiyo ya 13 mpaka sasa kalne ya 21.

Akizungumza na Mtandao huu kwenye mahojiano maarumu Mzee Mohamed Pazzi[80] Mkazi wa kijiji hicho,alidai kwamba toka azaliwe miaka 80 iliyopita kwenye kijiji hicho hajashuhudia maji hayo yakipungua au kuongezeka.

" Mimi nimezaliwa hapa miaka 80 iliyopita sijashuhudia maji haya wakipungua au kuongezeka toka karne hiyo ya 13,ambapo toka kipindi hicho mvua nyingi zimenyesha lakini hajaongezeka pia jua kali la toka kipindi hicho cha kalne ya 13 mpaka sasa alijaweza kukausha hata tone la maji hayo huku makundi ya watu wakichota maji hayo kila siku lakini pia hayajapungua"alisema Mzee huyo

Vile vile mzee huyo alieleza maajabu mengine yaliopo kwenye msakiti huo alidai kwamba kwa maelezo ya mababu zake Msikiti huo ulikuwa wa maajabu ambapo Sheikh aliyekuwa akiazini alipanda juu ya ngazi hizo na kuazini bila kipaza sauti lakini sauti yake ilifika umbali mrefu.

" Mababu  na mabibi zetu walitueleza kwamba Muazini alikuwa akipanda juu ya ngazi hizi alipoazini swara ile ya alfajiri sauti yake ilifika mbali sana kutoka eneo hili hadi Chalinze wakati mwingine sauti ilifika mikoa ya jirani kama Morogoro na Dar es salaam, wazee hao waliongeza kusema kwamba Sheikh aliazini bila kipaza sauti lakini kwa uwezo  wa Mwenyezi Mungu subuhana wa taara sauti hiyo ili peperushwa na upepo na kufika maeneo hayo ya mbali"aliongeza kusema Mzee Pazzi.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...