Hitmaker
wa Sorry, Barnaba amerekodi wimbo na msanii nguli wa Burundi aishiye
nchini Kenya, Kidum uliofanyika jijini Nairobi, Kenya chini ya producer
Kelly.
Wimbo huo uitwao Wamama umerekodiwa kwa udhamini wa benki ya Barclays
ambayo ni miongoni mwa wadhamini wa kampeni ya Montage Charity Ball
2013’ iliyoanzishwa na Teddy Mapunda kwaajili ya kukusanya fedha
kusaidia afya za wanawake.
Barnaba ameiambia Bongo5 kuwa gharama ya kurekodi wimbo huo pamoja na
malipo yao, usafiri na malazi ni zaidi ya shilingi milioni 25.
Amesema moyo wake wa kujitolea katika masuala ya kijamii, ni sababu
kubwa ya kuchaguliwa na kampuni ya Montage Limited kurekodi wimbo huo.
“Nimeamua kuimba kuhimiza watu kuchangia afya za akinamama kwasababu
mama anapokuwa vizuri basi kizazi cha mama ama mtoto pia naye atakuwa
vizuri,” amesema Barnaba.
Msikilize zaidi hapa.