Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Friday, May 10, 2013

Exclusive: Barnaba amshirikisha Kidum kwenye wimbo uliodhaminiwa na Barclays Bank – ala shavu la mil 25

Hitmaker wa Sorry, Barnaba amerekodi wimbo na msanii nguli wa Burundi aishiye nchini Kenya, Kidum uliofanyika jijini Nairobi, Kenya chini ya producer Kelly.
kidumu na barnaba
Wimbo huo uitwao Wamama umerekodiwa kwa udhamini wa benki ya Barclays ambayo ni miongoni mwa wadhamini wa kampeni ya Montage Charity Ball 2013’ iliyoanzishwa na Teddy Mapunda kwaajili ya kukusanya fedha kusaidia afya za wanawake.
Barnaba ameiambia Bongo5 kuwa gharama ya kurekodi wimbo huo pamoja na malipo yao, usafiri na malazi ni zaidi ya shilingi milioni 25.
Amesema moyo wake wa kujitolea katika masuala ya kijamii, ni sababu kubwa ya kuchaguliwa na kampuni ya Montage Limited kurekodi wimbo huo.
“Nimeamua kuimba kuhimiza watu kuchangia afya za akinamama kwasababu mama anapokuwa vizuri basi kizazi cha mama ama mtoto pia naye atakuwa vizuri,” amesema Barnaba.
Msikilize zaidi hapa.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...