Mstahiki
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akizungumza na waandishi wa
habari katika Hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam kuhusiana
na mfuko wa Ilala “Mayors Ball” kwa ajili ya kuchangisha fedha za
kununulia madawati kwa shule za msingi na sekondari zilizopo ndani ya
Manispaa ya Ilala. Katikati ni Afisa Elimu Msaidizi upande wa Takwim
Manispaa ya Ilala Wema Kajigile na kushoto ni Afisa Uhusiano wa Manispaa
ya Ilala Bi. Tabu Shaibu.
-Kauli mbiu ni Kalisha mmoja, boresha Elimu.
Msimu
wa mfuko wa uchangishaji wa Mayors ball una nia ya kuwa alama ya Meya
wa Ilala kwa kuwaleta pamoja viongozi wa idara mbalimbali Tanzania
katika tukio moja kwa dhumuni la kusaidia na kuhudumia jamii.
Madhumuni
ya waanzilishi wa mfuko wa Ilala Mayors Ball ni kujikita katika
uchangishaji wa fedha ambazo zitatumika kuwasaidia wakazi wa Ilala moja
kwa moja. Michango ambayo itakusanywa katika kila msimu wa mfuko wa
Mayor’s ball itakabidhiwa kwa vituo ambavyo vitakuwa vimependekezwa
katika kila msimu kupitia maombi maalumu.
“Kwenye
kila taifa llililoendelea kuna watu walioelimika. Ili kutengeneza
mazingira mazuri ya utoaji elimu kwa watoto wetu na taifa lijalo, vitu
mbalimbali ni muhimu kimoja wapo ikiwa ni dawati, hivyo basi kwa
kushirikiana na taasisi mbalimbali na jamii nzima kwa ujumla katika
msimu wa Mayor’s ball mwaka huu tutahakikisha kwamba wanafunzi wa
manispaa ya Ilala wanakaa kwenye madawati”. Hayo yamesemwa na Mheshimiwa
Jerry Silaa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala wakati akizindua kampeni
hiyo katika hoteli ya Hyatt Kilimanjaro tarehe 17 Mei 2013.
Mwaka
huu mradi wa mayor’s ball ambao imepewa jina la “Dawati ni Elimu”
inakuja na kauli mbiu isemayo “Kalisha mmoja, boresha Elimu.”
Mayor’s
ball mwaka huu imekusudia kuchangia shilingi Bilioni 4.98 kwa ajili ya
madawati katika shule za msingi na sekondari 30,487 za manispaa ya Ilala
ifikapo mwisho wa mwaka wa fedha 2013/14.
“Kwa
ajili ya kujenga mfuko wa Mayor’s ball kutakuwa na matukio mbalimbali
kama vile mechi za mpira wa miguu, matamasha ya muziki, maonesho ya
mavazi na matembezi ambayo yatajumuisha watu wa kaliba mbalimbali katika
jamii kama moja ya juhudi za kuunga mkono mfuko wa uchangishaji.”
Alisema Mustafa Hassanali mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya 361
Degrees ambayo imebuni na kusimamia mikakati na mchakato mzima wa mradi
huo kwa ajili ya ofisi ya Meya ikiwa ni sehemu ya mpango wa mahusiano ya
kikazi baina ya pande hizo mbili.
Mpaka
sasa kuna madawati 55,755 ambayo yanatumika kati ya madawati 86,242
ambayo yanahitajika. Hivyo basi kuna upungufu wa madawati asilimia
35.35, ili kuweza kukabiliana na upungufu huu inatakiwa kuundwa kampeni
za kijamii ambapo basi kila mmoja ataweza kuchangia kiasi chake ili
kuweza kuzipatia madawati shule katika manispaa ya Ilala.