Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Friday, April 19, 2013

TAMKO LA MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA TCRA KUHUSU USAJILI WA NAMBA ZA SIMU

13
Mkurugenzi wa Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) Prof John Nkoma akitoa hotuba katika mkutano wa kujadili  juu ya usajili wa namba za simu za mkononi .
Mkurugenzi wa Vodacom Rene Meza, naye akisisitiza jambo juu ya laini za simu
Prof. Nkoma katika mkutano huo alisema kwa kushirikiana na makampuni ya simu watumiaji wote wa simu za mkononi ambao hawajasajili namba zao wafanye hivyo mara moja, kwani utaratibu unaofuata ni kufunga namba zote ambazo hazijasajiliwa.
Akifafanua zaidi juu ya msimamo huo Nkoma alisema ni kosa la jinai kutumia namba ya simu isiyosajiliwa na adhabu yake ni faini ya shilingi laki tano au kifungo cha miezi mitatu jela.
Aidha amewataka  wananchi kuhakiki usajili wao kwa kupiga nyota 106 alama ya reli, ili kujua kama wamesajiliwa. 
  mkutano huo ulifanyika makao makuu ya mamlaka  ya mawasiliano Tanzania(TCRA) jijini Dar es salaam.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...