Blogger Widgets

Social Icons

Pages

Saturday, July 13, 2013

SIKU YA MASHUJAA KUFANYIKA MKOANI KAGERA

JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
 
11 Julai, 2013

Taarifa kwa Vyombo vya Habari
 
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linaadhimisha siku ya mashujaa kila tarehe 25 Julai, ikiwa ni sehemu ya kuwakumbuka mashujaa waliopigana na kushinda vita ya Kagera mwaka 1978/1979.

Maadhimisho hayo hufanyika mara moja kwa mwaka, na mwaka huu yatafanyika tarehe 25 Julai 2013 katika mkoa wa Kagera wilaya ya Bukoba kwenye makaburi ya mashujaa yaliyopo Kaboya.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo atakuwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. JAKAYA MRISHO KIKWETE.

Sambamba na mgeni rasmi, watakuwepo viongozi waandamizi wa Serikali, vyombo vya Ulinzi na Usalama, vyama vya siasa, taasisi za dini na taasisi mbalimbali za kiraia.

Vyombo vya habari vinaalikwa kushiriki katika maadhimisho hayo ambayo ni muhimu kwa Taifa.

Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
SLP 9203, Simu: 0764742161

Email: ulinzimagazine@yahoo.co.uk

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...